Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, November 18, 2014

SHULE YA MSINGI UJAMAA MJINI NJOMBE YAANZA KUTOA CHAKULA CHA MCHANA SASA

Hatimaye Shule Ya Msingi Ujamaa Imeanza Kutoa Chakula Cha Mchana Kwa Wanafunzi Baada ya   Afisa Elimu wa  Shule za Msingi za Halmashauri ya Mji wa Njombe  Zegeli Shengelo Kwenda Kufanya Mazungumza na Viongozi wa Shule  na Mtaa huo Kuhusiana na Utoaji wa Chakula Hicho.

Hatua Hiyo Ya Afisa Elimu  Wa Shule Za Msingi Wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Mwalimu Shengelo Imekuja Ikiwa Ni Siku Chache  Baada Ya Kituo Cha  Matangazo Cha Uplands Fm Radio  Kuarifu Kuwa  Shule  Ya Msingi Ujamaa Haitoi Chakula Cha Mchana Kwa Muda Wa Wiki Mbili  Kutokana Na Wazazi Kushindwa Kuchangia Chakula Hicho.

Wakizungumza Na Mtandao huu Baadhi Ya Wazazi Wenye Watoto Katika Shule Hiyo  Wamesema Sababu Ya Kushindwa Kuchangia Chakula Cha Mchana Kwa Wanafunzi wa Shule Ya Msingi Ujamaa Ni kutokana Na Mgongano  Wa Kimaslahi  Kwa Baadhi Ya Viongozi Wa Mtaa Na Kamati Ya Chakula  Kushindwa Kuaminiana Katika Ukusanyaji  Wa Chakula Kwa Wazazi.

Akizungumza ofisini kwake Mwenyekiti Wa Kamati Ya Chakula Katika Shule Ya Msingi Ujamaa Bwana Winfred Kayombo Amekili Shule Hiyo Kuanza Kutoa Chakula Cha Mchana  Baada Ya Afisa Elimu  Wa Shule Za Msingi Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Kuzungumza Nao  Na Kufikia  Uamuzi Wa Wazazi Kuanza Kuchangia Chakula Hicho Ambacho Kinaendelea Kuchangiwa Hadi Sasa. 

 Afisa Mtendaji Wa Mtaa Wa Kibena Hospitali  Bi.Kolumba Msemwa  Amesema Jitihada  Za Serikali Ya Mtaa Huo Zimeendelea  Kufanyika Baada Ya Afisa Elimu Zegeli Shengelo Kutoa Agizo La kutolewa Chakula Hicho Ambapo Serikali Ya Mtaa Huo imeamua Kuwafuata  Na Askali Mgambo  Baadhi ya Wazazi Wasiyopenda Kuchangia Chakula Hicho   Na Kwamba Kwa Watakaoshindwa Watafikishwa Katika Vyombo Vya Sheria.

No comments:

Post a Comment