Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, May 20, 2015

MABOMU YALINDIMA KILA MJINI NJOMBE. NI BAADA YA WANANCHI KUANDAMANA KUPINGA POLISI KUUA RAIA MAGARI YAZUIWA, MADUKA YAFUNGWA.

Wananchi Wakiwa  Barabarani Wakielekea Kibena  Wakiwa Kwenye Maandamano Makubwa Kuelekea Kibena Hospitali Kuangalia Mwili Wa Marehemu Pamoja Na Majeruhi

 WANANCHI WAKIELEKEA HOSPITALI YA KIBENA KWA MAANDAMANO  HUKU  WAKIIMBA NYIMBO


 MSURURU WA MAGARI BAADA YA KUONA WANANCHI WAKO MBELE NA BARABARA IMETAWALIWA NA WAO WENYEWE
HAPA WAPO  KITUO CHA DARADARA KIBENA HOSPITALI
HAPA NI HOSPITALI YA KIBENA  AMBAPO WANANCHI WAMEFIKA NA KUINGIA KWENYE WODI YA WANAUME NA KUMUANGALIA MAJERUHI ALIYEDAIWA KUPIGWA RISASI

HUYU NDIYE MAREHEMU  Basilius Ngore  Ambaye Amedaiwa Kufariki Kwa Kupigwa Risasi Na Watu Wanaodaiwa Kuwa Ni Askali Wa Polisi Enzi Za Uhai Wake   Alikuwa Fundi Ujenzi

HALI iLIKUWA HIVI KWENYE KITUO CHA DARADARA KIBENA KARIBU NA HOSPITALI YA KIBENA  WANANCHI WAMEKUSANYIKA WAKIWA HAWAELEWI KINACHOENDELEA  HUKU WENGINE WAKIWASHA MOTO BARABARANI KWENYE MOSHI UNAOONEKANA HUO.

KIKOSI CHA ASKALI WA POLISI  WAKIWA KWENYE MARI YAO  HUKU WANANCHI WAKIWATAZAMA KWA HASIRA KWA KUWA NDUGU ZAO  MMOJA KAPOTEZA MAISHA NA MMOJA KARAZWA HOSPITALI KWA KUJERUHIWA.




JAZBA ZA WANANCHI ZA SABABISHA KUWASHA MOTO BARABARANI KWA KUFUNGA BARABARA
HAPA NI ENEO LA  MTO RUHUJI  NJIAPANDA YA BARABARA YA MAKETE  ,MAKAMBAKO NA NJOMBE  WANANCHI PIA WAFUNGA BARABARA KWA MAWE  NA KULILAZIMU JESHI LA POLISI KUTUMIA NGUVU KUBWA YA KULIPUA MABOMU KUWATAWANYA.
BIASHARA NYINGINE ZILIKUWA ZIKIENDELEA MAENEO YA KITUO KIKUU CHA MABASI NJOMBE MJINI  LAKINI HALI YA TAHARUKI IKAANZA BAADA YA KUANZA KUFUNGWA BARABARA YA NJOMBE  SONGEA  ENEO LA STENDI YA NJOMBE MJINI
HUYU NI MAJERUHI FRED SANGA AMBAYE AMELAZWA KATIKA HOSPITALI YA KIBENA KWA MATIBABU ZAIDI BAADA YA KUDAIWA KUPIGWA NA RISASI
HAPA NI KIBENA WENGINE WAMEKAA KATIKATI YA BARABARA YA LAMI HAKUNA MAGARI KUPITA

HUU NI MSURURU WA MAGARI  WAKATI WA MAANDAMANO YA WANANCHI HAO









WAANDISHI WA HABARI WATATU WANAOONEKANA MBELE YAKO HUKU WALIKO MBELE WANAOPANDISHA BARABARA YA KUSHOTO NI WANANCHI WANAELEKEA BARABARA YA KUELEKEA MAKETE WANAKIMBIA MABOMU YANAYORIPULIWA NA ASKALI WA POLISI.

Njombe.
Hali ya tahaluki jana ilitanda  kwa wakazi wa Mji wa Njombe kufuatia kusikika milio ya mabomu kila kona baada ya polisi wa doria juzi usiku kuua raia mmoja kwa kumpiga risasi na kujeruhi mwingine katika klabu cha pombe cha Nyondo Mtaa wa Kambarage.
Kitendo hicho kilisababisha wananchi kuandamana hadi hospitali ya Mkoa wa Njombe Kibena anapotibiwa majeruhi huyo pamoja na kuhifdhiwa mwili marehemu.
Wananchi hao walisema wanaandamana ili kupinga mauji ya askari dhidi ya raia.
Aliyeuawa katika tukio hili ni Basil Ngole mkazi wa Mtaa wa Kambarage na aliyejeruhiwa ni Fred Sanga mkazi wa mtaa huo ambapo kwa sasa amelazwa katika hospitali hiyo.
Kufuatia tukio hilo wananchi walikusanyika hospitalini hapo majira saa moja asubuhi kupinga polisi kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia, huku wakipaza sauti za kulitaka jeshi la polisi kugharamia mazishi ya marehemu pamoja na matibabu ya aliyejeruhiwa.
Kutokana na kadhia hiyo polisi walifika eneo la tukio na kuanza kuwatawanya waandamanaji hao kwa mabomu ya machozi na kupelekea mwananchi mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Mandele dereva wa bodaboda mjini Njombe kujeruhiwa.
Kitendo hicho kiliamsha hasira kwa wananchi na kuanza vurugu kuziba barabara na mawe na kuchoma mataili ya gari barabarani.
Wakizungumzi tukio hilo baadhi wa wananchi mjini hapa, walilaani kitendo cha polisi kutumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia wasiokuwa na hatia, huku wakiomba askari aliyetekeleza mauaji hayo na majeruhi kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
Emanuel Filangali mkazi wa Njombe alisema hata kama marehemu na majeruhi na raia wengine walikuwa na kosa la kunywa pombe nje ya muda katika klabu hicho walipaswa kukamatwa na siyo sakari kuwapiga risasi na kusababisha kifo pamoja na majeruhi.
“Imekuwa kawaida kwa polisi kutumia nguvu kubwa dhidi ya raia, kama wao ndio wanashiriki kuua raia badala ya kuwalinda na mali zao kama ilivyosheria za jeshi la polisi, sasa wanafanya kazi gani,” alisema Emmanuel Ngalime.
Robert Shemajabu mkazi wa Njombe, alilitaka jeshi la polisi kuchukua jukumu la kumzika marehemu na kuwatibu majeruhi wa vurugu hizo na kuiomba serikali kumchukulia hatua kali askari aliyehusika na tukio hilo.
“Wananchi tumechoka dhuluma dhidi ya polisi walahi tunataka amani, lakini vitendo vy polisi kuendelea kuua raia havikubaliki hata kidogo, ni lazima jeshi la polisi litende haki kwa kuuzika mwili wa marehemu na kuwatibu waliojeruhiwa katika tukio hili, pili tunaomba askari aliyeua sheria ichukue mkondo wake maana hakuna mtu aliye juu sheria,” alisema Shemabu na kuongeza.
“Kama huyu askari hakutumwa kutenda haya aliyoyatenda na imani haki itatendeka, hatutaki kuona wakipindisha sheria mpaka sasa hivi hawataki kumtaja askari aliyeua,” alisema. 
 
Diwani wa Kata ya Njombe Mjini Agrey Mtambo alifika eneo la tukio na kuwaomba wananchi kudai haki yao lakini pia akiwataka kulinda usalama wao.
“Katika mazingira kila mmoja wetu aidai haki hii lakini pia akilinda usalama wake, tunachotaka hawa askari walioua nao wawajibishwe kwa mujibu wa sheria za nchi hii,” alisema Mtambo na kuongeza.
 “Tungeweza kuchanga kwa ajili ya mazishi na kumhamisha mgongwa lakini hatuwezi kufanya hivyo maana hili jukumu ni polisi waliotekeleza haya na RPC (Kamanda wa Polisi Mkoa) tumeshamueleza,” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Franco Kibona alipofuatwa na waandishi wa habari kutolea ufafanuzi suala hilo alisema kwa kifupi; “siwezi kuzungumzia suala hili kwa sasa wakati hali haijatulia”.
Hata hivyo alifika eneo la tukio na kuwasihi wananchi kutulia kwani madai yao yanashughulikiwa.
Hadi Mwandishi wa gazeti hili anatoka eneo la tukio majira ya saa tisa alasiri Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ilikuwa inaeendelea na kikao cha kujadili hali hiyo, huku hali ya usalama ikiwa haijatulia kwani mabomu ya machozi yalikuwa yakiendelea kusikika kuwatawanya waandamanaji waliokuwa na chupa za maji kukabiliana na mabomu ya machozi.
  
Hali hiyo tahaluki ilisababisha maduka mjini Njombe kufungwa, wafanyabiashara wakihofia hali ya usalama, huku waandamanaji wakiziba barabara kwa mawe kuzuia magari  na kuchoma mataili barabarani hali iliyopelekea magari ya polisi kuzunguka kila kona huku wakirusha mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji. 
Kwa Upande wake Majeruhi wa tukio hilo Fred Sanga akizungumza kwa taabu katika Hospitali ya Kibena anakopatiwa aliliambia gazeti hili kuwa, wakati akiwa katika klabu hicho askari polisi wa doria ambao hawakujalia sare za jeshi waliingia klabuni hapo na kuwaamuru yeye pamoja na wateja wengine wakae chini hali iliyozua mzozo.
Alisema kufuatia hali hiyo polisi walilazimika kufyatua risasi ambazo zilimpata yeye na marehemu, ambapo yeye alijeruhiwa sehemu za siri na makalio.
Katika eneo la polisi mwandishi wa gazeti hili alishuhudia baadhi ya raia wakishushwa kwenye gari la polisi kutokana na vurugu hizo na kuwekwa ndani. Huku kukiwa taarifa za kuvunjwa kwa nyumba ya askari mmoja anayedaiwa kutekeleza tukio hilo ambaye hakuweza kufahamika, ingawa wakazi wa Mtaa wa Kambarage walikuwa wakimtaja kwa jina la Jack.
........END.

No comments:

Post a Comment