Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, July 13, 2018

UJENZI WA HOSTEL YA SHULE YA SEKONDARI MTIMBWI KATA YA UTENGULE MJINI MAKAMBAKO WAANZA

 WANANCHI  WA  KIJIJI  CHA  NGAMANGA  KATA  YA  UTENGULE  WAKIWA  KWENYE  MKUTANO  WA  KUJADILI  UJENZI  WA  HOSTEL  HIYO  KUPUNGUZA  MIMBA  KWA  WANAFUNZI  .


 AFISA  MTENDAJI   WA  KATA  JOB  FUTE  AKIHIMIZA  WANANCHI  KUCHANGIA  UJENZI  HUO.

KAMPENI YA FURAHA YANGU KUZINDULIWA JUMANNE MKOANI NJOMBE

 

 MKUU   WA  MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  AKIZUNGUMZA NA  WAANDISHI   WA  HABARI  KUHUSIANA  NA  KAMPENI  YA  FURAHA  YANGU NJOMBE.

 MKUU   WA  MKOA  WA  NJOMBE  OLE SENDEKA  AKIWA  NA  WATALAAMU  WA  AFYA  MKOA  WA  NJOMBE.








Monday, May 21, 2018

JESHI LA POLISI MKOA WA NJOMBE LA MSHIKILIA KIJANA MMOJA ALIYEJIFANYA IGP SIRRO KUTAPELI WANANCHI

 KAMANDA  WA  JESHI LA  POLISI  MKOA  WA  NJOMBE  SACP RENATA MZINGA  AKIWAONESHA  WAANDISHI  MTUHUMIWA  HUYO.




 MTUHUMIWA  ALIYEJIFANYA  IGP  SIRO  KUTAPELI  MALI  ZA  WANANCHI  NJOMBE  AKAMATWA  NA  POLISI  KWA  MAHOJIANO  ZAIDI.




HUYU NDIYE   MARICHA MARICHA  MNIKO  MWENYE  UMRI  WA  MIAKA  30  MKURYA  MKAZI  WA  TANDALA  MAKETE   AMBAYE  NI  DEREVA   AKIWA  CHINI  YA  POLISI  MKOA  WA NJOMBE.


Sunday, March 18, 2018

HABARI ZA WIKI NI BAADA YA MKUU WA MKOA KURUHUSU BAJAJI KUENDELEA NA KAZI MADEREVA WA DALADALA WAKATIKISA KIBERITI KAMA KIMEJAA LAKINI WAREJEA KAZINI WENYEWE.

 MKUU  WA  MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  AMESEMA  WAMILIKI  NA  MADEREVA  WA  DALADALA  WANATIKISHA  KIBERITI  KAMA  KIMEJAA  NA KUWAAMURU  WARUDI  BARABARANI  KWA  ATAKAYEGOMA  ATAFUTIWA  LESENI YA  BIASHARA  ZAKE  ZOTE MKOA  WA  NJOMBE 
 KWA  MSISITIZO  MKUBWA  WAKISIKILIZA  HOJA  ZA  WAMILIKI  ZA  KWAMBA  BAJAJI  HAWAKO  KISHERIA  JAMBO  AMBALO  MKUU  WA  MKOA  AMESEMA  HATEGEMEI  KUONDOA  USAFIRI  WA  BAJAJI  BARABARANI  ISIPOKUWA  KUONGEZA  45 ZIWE  100  DALADALA  WAOMBA  MSAMAHA  ASIONGEZE  NYINGINE .



 WAMILIKI  WA  DALADALA  MKOA  WA  NJOMBE  WAKIWA  KATIKA  KIKAO  NA MKUU  WA  MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  BAADA  YA  KUGOMA  KUFANYA  KAZI  MALALAMIKO  YAO  YAMESIKILIZWA  LAKINI  BADO  MAAMUZI  HAYAJACHUKULIWA  HADI  KAMATI  ALIYOIUNDA  MKUU  WA  MKOA  IKUTANE  NA  ASIWEPO  MTU WA KUFIKILIA  KUZIONDOA  BAJAJI  BARABARANI.






MADEREVA  DALADALA  WAKITOKA  NJE  BAADA  YA  MKUU  WA  MKOA  KUTOA  MAAMUZI  YAKE  SASA  WANATOKA  KWENDA  KUFANYA  KIKAO  CHAO CHA  KURUDI  BARABARANI.



NJOMBE

Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Christopha  Olesendeka  Amepiga  Marufuku  Kuwepo  Kwa  Migomo  Ya  Wamiliki  Wa  Usafiri   Aina  Yoyote  Ile  Kwamba  Kwa  Atakayebainika  Kufanya  Mgomo  Atafutiwa  Leseni  Ya  Biashara  Yake.

Kauli  Ya  Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Olesendeka  Imetolewa  Kufuatia   Wamiliki  Wa  Daladala  mjini Njombe  Kugoma  Kusafirisha  Abiria  Kushinikiza  Kuondolewa  Kwa  Usafiri  Wa  Pikipiki  Za  Magurudumu  Matatu  Maarufu  Kama  Bajaji  Ambazo  Zimeruhusiwa  Kuendelea Kutoa  Huduma  Hivi  Karibuni.

Olesendeka  Amesema  Kitendo  Walichofanya  Wamiliki  Wa  Magari  Aina Ya  Hice  Cha  Kugoma  Kufanya  Kazi  Hajaridhishwa  Nacho  Nakwamba   Atakayebaini   Kuendekeza  Migomo   Na  Maandamano   Hatua  Kali  Zitachukuliwa  Dhidi  Yake  Ikiwa  Ni  Pamoja   Na  Kufutiwa  Leseni Za  Biashara.

Baada  Ya  Mkuu  Wa  Mkoa  Kusema  Asiwepo  Mtu  Yeyote  Atakaye Kuwa  Na Mawazo  Ya  Kuziondoa  Bajaji  Barabarani  Mwenyekiti  Wa  Wamiliki  Wa  Daladala  Peter  Haule  Ameshukuru  Kwa  Maamuzi  Na Kusema  Wako  Tayari  Kufuata  Utaratibu  Utakao Kuwepo.


Nao  Wamiliki  Wa  Daladala  Walipopewa  Nafasi  Ya  Kutoa  Maoni  Na Mapendekezo  Yao  Wamesema  Bajaji  Zinawamalizia  Abiria  Wote  Walioko  Mjini  Ikiwa  Wao   Wanasafiri  Umbari  Mrefu  Wa  Kilomita  18  Kwa  Shilingi  Mia  Nne Huku  Bajaji  Wanasafiri  Umbali  Wa  Kilomita  Tatu  Kwa  Shilingi  Mia  Tano  .

  Daladala  Zimeamuliwa  Kuendelea  Na  Kazi  Hadi  Mwafaka  Wao  Na  Bajaji  Na Bodaboda  Utakapo  Patikana   Bila  Kuwepo  Mtu  Wa  Kushindwa  Kufanya  Kazi  Ya  Kutoa  Huduma  Ya  Usafiri  Kwa  Abiria  Katika  Maeneo  Yao.


RC NJOMBE AREJESHA BAJAJI BARABARANI, DALADALA WAKASILIKA

WAMILIKI  NA  MADEREVA  WA  BODABODA  NA  BAJAJI  WAKIWA  KWENYE  MKUTANO  WA  KUREJESHWA  KWA  BAJAJI  BARABARANI






MKUU  WA  MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  AKIWASILI  KATIKA  UKUMBI  WA  TURBO  MJINI  NJOMBE  KUWASIKILIZA  KERO  MADEREVA  NA  WAMILIKI  WA  PIKIPIKI  ZA  MAGURUDUMU  MAWILI  NA  MATATU  BAJAJI

TAZAMA  MABANGO  MBALIMBALI  YA  KERO  HAPA  CHINI NI KERO  ZA  BODABODA  NA  BAJAJI ZIKIWASILISHWA  KWA  MKUU  WA  MKOA  WA  NJOMBE.














NJOMBE

Hatimaye  Sakata  La  Kuzuiliwa  Kwa   Bajaji  Zisifanye Kazi  Katika  Barabara  Kuu Limepatiwa  Ufumbuzi  Na Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Christopha  Ole  Sendeka  Baada  Ya  Kuruhusu  Bajaji  Hizo  Kuendelea  Kufanya  Kazi  Kama Kawaida.

Ole Sendeka  Pia  Ameruhusu  Wamiliki  Wa Bajaji  Na Wadau  Wengine  Wa  Usafiri  Kuongeza   Bajaji  Nyingine  Arobaini  Na  Tano   Ili  Kufikisha  Idadi  Ya  Bajaji  100  Tofauti  Na  Ilivyo  Kwa  Sasa  Ambapo  Bajaji   55 Pekee  Ndizo  Zinazofanya  Kazi.

Bwana  Sendeka  Amesema  Ofisi  Yake  Ipo Wazi  Kuanzia  Sasa  Kwaajili  Ya  Kusikiliza  Malalamiko  Na  Kero  Za  Madereva  Bodaboda  Na  Bajaji  Na  Kuagiza  Kuwa  Asiwepo  Kiongozi  Yeyote  Wa Kuwasumbua   Kwa  Kuwataka  Wapaki  Nje  Ya Mji  Siwepo  Hali  Hiyo.

Katika  Hatua  Nyingine  Sendeka  Ametumia  Fursa  Hiyo  Kukemea  Tabia  Ya  Kufanya  Maandamano  Yasiyo  Rasmi  Na  Kusema  Vijana  Wasijaribu  Kufanya  Kazi  Hiyo  Kwani   Serikali  Haitalifumbia  Macho  Swala  Hilo.

Awali    Mwenyekiti  Wa  Bajaji  Barnaba  Mwangi  Amesema  Changamoto  Kubwa  Wanayokabiliwa  Nayo  Ni  Kufukuzwa  Kwenye  Barabara  Kuu  Na  Wanaosababisha  Ni  Wamiliki  Wa  Dalala Ambao  Wanataka  Wafanye  Wao  Biashara  Ya  Kusafirisha  Abiria  Huku Mwenyekiti Bodaboda  Filemon  Mwinuka Naye  Akilia  Na  Tozo  Mbalimbali Zinazotozwa.

Kwa  Upande  Wao  Wamiliki  Wa  Bajaji  Wakizungumza  Kwa  Fuaha  Wamemshukuru  Mkuu  Wa  Mkoa  Kwa  Juhudi  Alizofanya    Na  Kusema  Amejali  Huduma  Zinazotolewa  Na  Vyombo  Hivyo  Na  Kutaka  Viongozi  Wengine  Kuiga  Mfano  Huo.