Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, June 30, 2016

TAKUKURU NJOMBE YAKAMATA WATUMISHI WAKE WAWILI WALIOOMBA RUSHWA YA LAKI SITA WILAYANI MAKETE

 KAMANDA WA TAKUKURU MKOA WA NJOMBE CHARLES NAKEMBETWA AKIWA OFISINI KWAKE AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI



Taasisi Ya Kuzuia Na Kupambana Na Rushwa Mkoa Wa  Njombe  Inawashikilia Watumishi Wake Wawili Wa Wilaya Ya Makete  Kwa Tuhuma Za Kuhusisha Na Ufisadi Na Kuomba Rushwa  Ya Shilingi Laki Sita Kwa Mwananchi   Jina Lake  Limehifadhiwa  Kwa Usalaama Wake Ambaye Alikuwa Anakabiliwa Na Tuhuma Za Kugushi Vyeti  Vya Ajira  Wilayani Humo.

Akizungumza Na Waandishi Wa Habari Ofisini Kwake Kamanda Wa Takukuru Mkoa Wa Njombe Charles Nakembetwa Amewataja Watuhumiwa Hao Kuwa Ni Pamoja Na  Mwanasheria Wa Taasisi Ya Takukuru Wilaya Ya Makete Frednand  Nsakuzi Pamoja Na Mlinzi  Wa Ofisi Ya Takukuru Makete Julius  Hasani  Wote Watumishi Wa Taasisi Ya Kuzuia Na Kupambana Na Rushwa Wilani Makete.

Kamanda Nakembetwa Amesema Watuhumiwa Hao Kwa Pamoja  Waliomba Kiasi Hicho Cha Fedha Shilingi Laki Sita Kwa  Mwananchi Ambaye Jina Lake Limehifadhiwa  Katika Tukio Lililotokea    June 28  Mwaka Huu Majira Ya  Saa Moja Na Saa Mbili Usiku  Ambapo Waliomba Rushwa  Kwa  Mwananchi Huyo Aliyekuwa Anatuhumiwa Kugushi Vyeti Vya Ajira.

Charles Nakembetwa Ameiambia Uplands Fm Kuwa  Watuhumiwa Hao  Walifanikiwa Kupokea Fedha Ya Awali Shilingi Laki Moja   Ambapo  Baada Ya Takukuru Mkoa Wa Njombe Kupata Taarifa Hizo Walifanikiwa Kulia Doria Na Kuwakamata  Wahusika Wakiwa  Wanachukua Fedha Hizo Kinyume Na Kifungu Cha  15 Cha Sheria  Ya Kuzuia Na Kupambana Na Rushwa Namba 11  Ya Mwaka 2007.

Amesema Watuhumiwa Hao Walitenda Kosa Hilo Kinyume Na Sheria Ya Makosa Ya Jinai  Na Kosa La Kutoa Siri Za  Ofisi  Wakiwa Watumishi Wa Umma Na Kwamba Taratibu Za Kuwasimamisha Kazi Zinaendelea  Ikiwa Ni Pamoja Na Kuwafikisha Mahakamani  Kujibu Tuhuma Zinazowakabili  Mara Baada Ya Uchunguzi Kukamilika.

Aidha Takukuru Mkoa Wa Njombe Imewashukuru Baadhi Ya Wananchi Wanaoendelea Kuonesha Ushirikiano Huo Wa Kutoa Taarifa  Za Vitendo Vya Rushwa  Vinavyoendelea Kufanyika Miongoni Mwa  Viongozi  Wa Serikali Na Watu Binafsi Kwani Vindo Hivyo Vitatokomezwa Endapo Wananchi Wataonesha Mshikamano Huo.

No comments:

Post a Comment