Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, July 1, 2013

MUHASHAMU ASKOFU WA JIMBO LA LINDI BRUNO NGONYANI AMEZINDUA KONGAMANO LA UTOTO MTAKATIFU LINALOFANYIKA JIMBO LA NJOMBE JANA..


 WATOTO WA KIPAPA WAKIWA KWENYE KONGAMANO HILO HAPO JANA
























 MUHASHAMU ASKOFU WA JIMBO LA LINDI AMBAE ALIKUWA MGENI RASMI HAPO JANA NA KUZINDUA KONGAMANO HILO LA WATOTO
 MAPADRE KUTOKA MKOA WA IRINGA
 MAPADRE WA JOMBO LA NJOMBE



 MUHASHAMU ASKOFU ALFRED  MALUMA AKIWASIHI WATOTO KUZINGATIA MAFUNZO WATAKAYOPEWA NA KUTUNZA MAADILI YA KIDINI


 MKURUGENZI WA VIJANA NA WATOTO  JIMBO LA NJOMBE PADRE CLEMENT MGOHELE  AKITOA NASAHA KWA WATOTO HAO

 MAPADRE WA KUTOKA JIMBO LA NJOMBE
MUHASHAMU  ASKOFU  WA JIMBO LA NJOMBE ALFRED  MALUMA AKIWA NA MUHASHAMU ASKOFU WA JIMBO LA LINDI BRUNO NGONYANI











 BAADA YA KUMALIZIKA KWA UFUNGUZI WA KONGAMANO HILO MUHASHAMU ASKOFU NGONYANI AKAANZA KUWASALIMU WATOTO KWA KUWASHIKA MKONO KILA MMOJA.PICHA NA MICHAELNGINGWA
Mhashamu Askofu wa Kanisa Katoliki  Jimbo la Lindi Bruno Ngonyani Leo Amezindua Kongamano la Siku Nne la Utoto Mtakatifu
Kwa Mikoa ya Kusini Ambapo amewataka Watoto Wanaoshiriki Kongamano Hilo Kuwa Mabalozi Katika Jamii Katika Kutenda Matendo ya Kumpendeza Mungu.

Akizungumza Wakati wa Kufungua Kongamano Hilo Askofu Ngonyani Ameseam Kongamano Hilo Litasaidia Kwa Kiasi Kikubwa Kuwajenga Watoto Hao Katika Imani ya Kidini na Maadili Mema Huku Akiwataka Watoto Hao Kuwa Wavumilivu Kwa Kipindi Chote cha Mafunzo Yatakayotolewa Kwenye Kongamano Hilo

Aidha Askofu Ngonyani Amewataka Viongozi wa Dini Wakiwemo Watawa na Mapadri Kutumia Kongamano Hilo Kuwafundisha Watoto Hao Elimu ya Dini Ukiwemo Utawa na Upadri Pamoja na Usomaji wa Biblia.

Askofu Ngonyani Amewapongeza Viongozi wa Kanisa Katoliki la Njombe Kwa Kuandaa Kongamano Hilo Linalowakutanisha Watoto Kutoka Mikoa ya  Njombe , Lindi Mbeya , Iringa na Ruvuma Ambalo Limelenga Kuwapa Mafunzo Mbalimbali ya Kidini na Jamii Inayowazunguka .

Akielezea Lengo la Kongamano Hilo Padre Clement Mgohele Ambaye ni Mkurugenzi wa Vijana na Watoto wa Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe Amesema ni Kutoa Semina Kwa Watoto Hao Juu ya Maadili Mema Katika Jamii na Mafundisho ya Maandiko Matakatifu Ikiwemo Kuyasoma na Kuyaelewa Maandiko Hayo.

Ameongeza Kuwa Kongamano Hilo Litasaidia kuwajenga watoto katika  Maadili Kwa Vijana Hasa Katika Kizazi Hiki Ambacho Vijana Wengi Wamejiingiza Katika Tabia na Matendo Maovu Yanayoshusha Maadili ya Mtanzania.

Zaidi ya Watoto Elfu Mbili wa Kikristo wa Kanisa Katoliki Kutoka Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini Wanashiriki Katika Kongamano Hilo la Siku Nne Mjini Njombe.

No comments:

Post a Comment