Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, April 11, 2016

CHUO CHA FUTURE WORLD VOCATION INSTITUTE CHATOA MAFUNZO YA UDEREVA KWA BODA BODA 111 NJOMBE


 Mratibu Wa Mafunzo  Ya Usalama Wa Barabarani  Kutoka Future World V.T.C  Yusto  Walisimba Akizungumza Na Wahitimu Hao

 ALAMA ZA BARABARANI WALIZOPEWA
 WAHITIMU WANATUNUKIWA VYETI VYA KUHITIMU MAFUNZO HAYO





 KAMANDA WA KIKOSI CHA USALAAMA BARABARANI MKOA WA NJOMBE KALVIN  NDIMBO AKIWA KWENYE HAFRA HIYO FUPI YA KUWATUNUKU VYETI WAHITIMU  WA MAFUNZO  YA UDEREVA


 MBWILO AKIPOKEA CHETI CHA MAFUNZO YA UDEREVA







 WAHITIMU WA MAFUNZO YA UDEREVA  WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MGENI RASMI KAIMU KATIBU TAWALA MKOA LAMECK NOA PAMOJA NA WAKUFUNZI KUTOKA VTC DAR ES SALAAM PAMOJA NA JESHI LA POLISI KUPITIA KITENGO CHA USALAMA BARABARANI.

Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi  Amewataka Madereva Wa Vyombo Vya Moto Hususani Madereva Bodaboda Kujitokeza Kwa Wingi Kupatiwa Mafunzo Na  Leseni Za Udereva   Ili Waweze Kufuata  Sheria Na Kanuni Za Barabarani   Na Kupunguza Matukio Ya Ajali Ambazo Zimekuwa Zikijitokeza Mkoani Njombe  Kwa Kukiuka Sheria Hizo.

Akizungumza Wakati Wa Kufunga Mafunzo Ya Udereva  Kwa  Wamiliki Na Madereva Wa Pikipiki 111   Kwa Niaba Ya Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi,Kaimu Katibu Tawala Mkoa Wa Njombe Lameck Noa  Amewataka Madereva Hao Kufuata Sheria Za Usalama Wa Barabarani  Kwa Kuacha Kuendesha Vyombo Vya  moto Kwa Mwendo Kasi Na Kuendesha Kwa Sifa.

Aidha Kaimu Katibu Tawala Huyo Noa Amesema  Sheria Na Alama Mbalimbali Za Barabarani  Madereva Hao Wameweza Kufundishwa    Na Wakufunzi Wa Kutoka Chuo Cha V.T.C Cha  Future World  Insititute  Cha Dar Es Salaam  Ikiwemo Sheria Na Kanuni Za Uendeshaji,Alama Za Barabarani, Kupunguza Mwendo Kasi Maeneo Mhimu Na Kutopiga Honi Maeneo Ya Mahakama Na  Hospitali.

Awali Akizungumza  Mratibu Wa Mafunzo  Ya Usalama Wa Barabarani  Kutoka Future World V.T.C  Yusto  Walisimba  Mkola  Ametaka Jeshi La Polisi  Kuhakikisha Linawakamata  Baadhi Ya Madereva Wote Wanaoendesha Vyombo Vya Moto  Huku Wakiwa Hawana Leseni   Kwani Ajali Nyingi Hapa Nchini Zinasababishwa Na Madereva Wazembe  Wasiyo Na Leseni.

Akisoma Risala Fupi Ya Washiriki Wa Mafunzo Ya Usalama  Barabarani  Na Polisi Jamii   Kwa Niaba Ya Washiriki Wengine  Jeniko Lusungu Mbwilo   Amesema Jumla Ya Wahitimu  111 Wa Kutoka Maeneo Mbalimbali  Ya Mkoa Wa Njombe Walihudhuria Mafunzo Hayo Lakini  Ni Wahitimu 62 Waliotunukiwa Vyeti  Vya  Udereva  Siku Ya Leo Kutokana Na Sababu Mbalimbali.

Mafunzo Hayo Yametolewa Na  Jeshi La Polisi  Mkoa Wa Njombe Kwa Kushirikiana Na  Chuo Cha Future  World  Vocation  Institute Kutoka Dar Es Salaam   Kwa Kuelimisha  Mambo Mbalimbali Wanayotakiwa Kuzingatia Madereva Wakiwa Kazini Kuwa  Ni Pamoja Na Kuzingatia Usafi  Na Ulinzi  Shirikishi Kwa Kuwafichuwa Waharifu Mbalimbali  Kwani Wao Ndiyo Wahusika Wa Kuwasafirisha Waharifu.
...............................................................................................................................................................................

1 comment:

  1. NI VIZURI KUSHIRIKI MAFUNZO ILI KUONDOA UJINGA WA BARABARANI

    ReplyDelete