Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, March 18, 2018

HABARI ZA WIKI NI BAADA YA MKUU WA MKOA KURUHUSU BAJAJI KUENDELEA NA KAZI MADEREVA WA DALADALA WAKATIKISA KIBERITI KAMA KIMEJAA LAKINI WAREJEA KAZINI WENYEWE.

 MKUU  WA  MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  AMESEMA  WAMILIKI  NA  MADEREVA  WA  DALADALA  WANATIKISHA  KIBERITI  KAMA  KIMEJAA  NA KUWAAMURU  WARUDI  BARABARANI  KWA  ATAKAYEGOMA  ATAFUTIWA  LESENI YA  BIASHARA  ZAKE  ZOTE MKOA  WA  NJOMBE 
 KWA  MSISITIZO  MKUBWA  WAKISIKILIZA  HOJA  ZA  WAMILIKI  ZA  KWAMBA  BAJAJI  HAWAKO  KISHERIA  JAMBO  AMBALO  MKUU  WA  MKOA  AMESEMA  HATEGEMEI  KUONDOA  USAFIRI  WA  BAJAJI  BARABARANI  ISIPOKUWA  KUONGEZA  45 ZIWE  100  DALADALA  WAOMBA  MSAMAHA  ASIONGEZE  NYINGINE .



 WAMILIKI  WA  DALADALA  MKOA  WA  NJOMBE  WAKIWA  KATIKA  KIKAO  NA MKUU  WA  MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  BAADA  YA  KUGOMA  KUFANYA  KAZI  MALALAMIKO  YAO  YAMESIKILIZWA  LAKINI  BADO  MAAMUZI  HAYAJACHUKULIWA  HADI  KAMATI  ALIYOIUNDA  MKUU  WA  MKOA  IKUTANE  NA  ASIWEPO  MTU WA KUFIKILIA  KUZIONDOA  BAJAJI  BARABARANI.






MADEREVA  DALADALA  WAKITOKA  NJE  BAADA  YA  MKUU  WA  MKOA  KUTOA  MAAMUZI  YAKE  SASA  WANATOKA  KWENDA  KUFANYA  KIKAO  CHAO CHA  KURUDI  BARABARANI.



NJOMBE

Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Christopha  Olesendeka  Amepiga  Marufuku  Kuwepo  Kwa  Migomo  Ya  Wamiliki  Wa  Usafiri   Aina  Yoyote  Ile  Kwamba  Kwa  Atakayebainika  Kufanya  Mgomo  Atafutiwa  Leseni  Ya  Biashara  Yake.

Kauli  Ya  Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Olesendeka  Imetolewa  Kufuatia   Wamiliki  Wa  Daladala  mjini Njombe  Kugoma  Kusafirisha  Abiria  Kushinikiza  Kuondolewa  Kwa  Usafiri  Wa  Pikipiki  Za  Magurudumu  Matatu  Maarufu  Kama  Bajaji  Ambazo  Zimeruhusiwa  Kuendelea Kutoa  Huduma  Hivi  Karibuni.

Olesendeka  Amesema  Kitendo  Walichofanya  Wamiliki  Wa  Magari  Aina Ya  Hice  Cha  Kugoma  Kufanya  Kazi  Hajaridhishwa  Nacho  Nakwamba   Atakayebaini   Kuendekeza  Migomo   Na  Maandamano   Hatua  Kali  Zitachukuliwa  Dhidi  Yake  Ikiwa  Ni  Pamoja   Na  Kufutiwa  Leseni Za  Biashara.

Baada  Ya  Mkuu  Wa  Mkoa  Kusema  Asiwepo  Mtu  Yeyote  Atakaye Kuwa  Na Mawazo  Ya  Kuziondoa  Bajaji  Barabarani  Mwenyekiti  Wa  Wamiliki  Wa  Daladala  Peter  Haule  Ameshukuru  Kwa  Maamuzi  Na Kusema  Wako  Tayari  Kufuata  Utaratibu  Utakao Kuwepo.


Nao  Wamiliki  Wa  Daladala  Walipopewa  Nafasi  Ya  Kutoa  Maoni  Na Mapendekezo  Yao  Wamesema  Bajaji  Zinawamalizia  Abiria  Wote  Walioko  Mjini  Ikiwa  Wao   Wanasafiri  Umbari  Mrefu  Wa  Kilomita  18  Kwa  Shilingi  Mia  Nne Huku  Bajaji  Wanasafiri  Umbali  Wa  Kilomita  Tatu  Kwa  Shilingi  Mia  Tano  .

  Daladala  Zimeamuliwa  Kuendelea  Na  Kazi  Hadi  Mwafaka  Wao  Na  Bajaji  Na Bodaboda  Utakapo  Patikana   Bila  Kuwepo  Mtu  Wa  Kushindwa  Kufanya  Kazi  Ya  Kutoa  Huduma  Ya  Usafiri  Kwa  Abiria  Katika  Maeneo  Yao.


No comments:

Post a Comment