Monday, April 14, 2014
MKUU WA MKOA WA NJOMBE KEPTAIN MSTAAFU ASERI MSANGI AAGIZA UTENGENEZAJI WA MADAWATI YA WATOTO WA CHEKECHEA NA SIYO WANAYOTUMIA KWA SASA
HAPA ANAANGALIA MADAWATI HAYO JINSI YALIVYOHARIBIWA PASIPO MATENGENEZO YOYOTE HII IMETOKEA BAADA YA KUFANYA ZIARA YA DHARULA KATIKA SHULE YA MSINGI ILUNDA KATA YA MTWANGO WILAYANI NJOMBE
MKUU WA MKOA AMELAANI KITENDO HIKI CHA MADAWATI KUHIFADHIWA VIBAYA MENGINE YAMEVUNJIKA NA KUWATAKA WAKUU WA SHULE KUYATUNZA MADAWATI HAYO
MKUU WA MKOA WA NJOMBE AKIKAGUA VITABU VYA MWALIMU MKUU WA SHULE YA MSINGI ILUNDA
HAYA NDIYO MAHINDI ALIYOPANDIA MBOLEA YA MNJINGU MAZAO MKUU HUYO WA MKOA WA NJOMBE
DANIEL NGALUPELA KATIBU WA MKUU WA MKOA WA NNJOMBE
MSANGI AKITOA UFAFANUZI JUU YA MAHINDI ALIYOYATUMIA KUPANDIA NA KUKUZIA MBOLEA YA MINJINGU MAZAO SHAMBA LAKE ALILOLIMA KIJIJI CHA ITIPINGI KAMA LA MFANO WA KUWAONESHA WANANCHI AMBAO WANAIKATAA MBOLEA HIYO
SHAMBA DARASA LA SOYA KIJIJI CHA ITIPINGI
AFISA MTENDAJI WA KIJIJI CHA ITIPINGI ASANGIE MANGULA AKISOMA TAARIFA FUPI MBELE YA MGENI RASMI
Mkuu wa mkoa wa Njombe keptain Mstaafu Aseri Msangi ameziagiza halmashauri za mkoa wa Njombe kutengeneza madawati kwaajili ya wanafunzi wa madarasa ya chekechea huku wananchi wakitakiwa kuchangia chakula shuleni ili kuboresha kiwango cha taaluma shuleni.
Akizungumza wakati wa kukagua mazingira ya shule ya msingi Ilunda Mkuu wa mkoa Keptain Mstaafu Aseri Msangi amewataka walimu kutunza samani zilizopo kwa kutengeneza ili kupunguza changamoto ya upungufu wa madawati inayozikabili shule nyingi za msingi mkoani Njombe.
Aidha Keptain Msangi amewapongeza wananchi wa kitongoji cha Lima kwale kwa ujenzi wa shule ya msingi Ilunda Mkondo B na kuwataka kukamilisha ujenzi wa madarasa na sehemu ya kupikia chakula cha wanafunzi huku akimuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Njombe Paulo Malala kuhakikisha anapeleka mwalimu mkuu wa kusimamia shule hiyo ili ifikapo july mwaka huu iweze kufunguliwa rasmi na kuanza masomo.
Katika hatua nyingine Keptain Msangi amewaondoa hofu wananchi mkoani hapa juu ya matumizi ya mbolea aina ya minjingu mazao kwa kuwataka wananchi kuepukana na kilimo cha mazoea na kwamba mbolea hiyo inafaa kwa kilimo cha mazao huku akitolea mfano shamba lake alilolima mwaka huu na kupandia mbolea hiyo katika kijiji cha Itipingi kuwa ametumia mbolea ya minjingu mazao na mahindi yameonekana kustawi vizuri.
Akisoma taarifa fupi mbele ya mkuu wa mkoa wa Njombe afisa mtendaji wa kijiji cha Ilunda bwana Yarabi Kafumbe amesema kuwa lengo la wananchi wa kijiji hicho kuanzisha shule hiyo ya mkondo B,Iliyopo kitongoji cha Limakwale katika shule ya msingi Ilunda ni kutaka kuwapunguzia wanafunzi kusafiri umbali mrefu kwani kwa sasa wanasafiri umbali wa kilomita takribani tano.
Aidha bwana Kafumbe amesema kuwa madarasa ya shule hiyo yamegharimu shilingi milioni kumi na tatu na laki tatu ambapo halmashauri ya wilaya ilichangia shilingi milioni kumi na moja na wananchi wakichangia shilingi milioni mbili na laki tatu huku akiwaomba wadau wa elimu kusaidia kuchangia ujenzi huo ili kuendelea kuboresha vyumba vingine vya madarasa na ofisi.
Ziara hiyo ya siku tatu ya Mkuu wa mkoa wa Njombe imelenga kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Hapa ambapo Jumla ya shilingi laki nne zimeahidiwa na mkuu huyo wa mkoa kwaajili ya kutengeneza madawati ya wanafunzi wa darasa la chekechea katika shule ya msingi Ilunda mkondo B ambayo yanalingana na umri wao ambapo leo ziara hiyo inaendelea kwa vijiji vya taraafa ya Lupembe.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment