Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, April 14, 2014

MKUU WA MKOA WA NJOMBE AANZA ZIARA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO


 WA KWANZA UPANDE WA KULIA NI MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE PAULO MALALA,WA PILI KUTOKA KULIA NI MKUU WA MKOA WA NJOMBE KEPTAIN MSATAAFU ASERI MSANGI,WA TATU NI MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE VALENCE KABELEGE NA WA NNE NI KATIBU TAWALA  MKOA WA NJOMBE JACKSON SAITABAU

 WAKUU WA IDARA MBALIMBALI TOKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE WAKIWA KATIKA UKUMBI WA HALMASHAURI HIYO

 AFISA HABARI MKOA WA NJOMBE CHRISTOPHA PHILEMON

 MKUU WA WILAYA YA NJOMBE SARAH DUMBA AKIWASILI KATIKA UKUMBI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE
 AFISA HABARI WILAYA YA NJOMBE LUKERO MSHAULA AKISIKILIZA KWA UMAKINI MGENI RASMI MKUU WA MKOA WA NJOMBE KEPTAIN MSTAAFU ASERI MSANGI





 MUHANDISI WA MAMLKA YA MAJI WILAYA YA NJOMBE

 AFISA ELIMU SEKONDARI AKITOA TAARIFA YA IDARA YA ELIMU SEKONDARI

Mkuu wa mkoa wa Njombe Captain msataafu Aseri msangi  amepokea taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya halmashauri Na za wakuu idara Wilaya ya Njombe taarifa iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo bwana Paulo Malala mapema  leo katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Akiwasilisha taarifa mbalimbali za utekelezaji wa miradi  mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Njombe   bwana Pulo Malala amesema  halmashauri imeendelea kuwezesha vikundi  vya vijana na wanawake ili wajikwamu na dimbwi la umasikini ambapo kwa kipindi cha mwaka 2012 na 2013  halmashauri ilitoa jumla ya shilingi milioni ishilini na nne kama mikopo yenye masharti nafuu kwa vikundi  24 vya wanawake.

Aidha bwana Malala amesema kuwa kati ya shilingi milioni ishilini na nne zilizotengwa kwa kipindi cha mwaka 2012 na 2013 shilingi milioni kumi na moja  zilitengwa kwaajili ya vijana  ambapo katika kipindi cha mwezi julai 2013 hadi machi  2014  halmashauri ya wilaya imeendelea na mchakato wa kuviandaa vikundi vya wanawake na vijana 32 kwaajili ya  kupatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni ishilini na nne.

Katika taarifa ya fedha iliyosomwa na mkuu wa Idara ya fedha Rhoda Mahava imeeleza mikakati  mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato katika vyanzo vilivyopo  ikiwemo halmashauri kufanya mapitio katika kipindi  cha mwezi april hadi june 2014 ,Halmashauri imebinafsisha ukusanyaji wa mapato katika kata ya Ikuna huku mchakato wa kubinafsisha magulio ya Kidegembye,Mtwango,Matembwe na Ikondo unaendelea.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya kwanza iliowasilishwa na idara ya Fedha mkuu wa mkoa wa Njombe Aseri Msangi amezitaka halmashauri kuweka mipango mikakati dhabiti ya ukusanyaji wa mapato ambapo wahusika wa kusimamia  ukusanyaji huo ni  watendaji wa vijiji.

Amesema kuwa ni vema halmashauri  za wilaya zihakikishe watendaji wote wa vijiji na kata wanaishi karibu na mahala pa kazi ili kurahisisha ukusanyaji mapato kwa urahisi zaidi na kwamba mkoa wa Njombe watendaji wengi hawaishi katika maeneo yao ya kazi.

No comments:

Post a Comment