Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, October 26, 2017

MVUA ZASABABISHA HUDUMA ZA USAFIRI BARABARA YA MOROGORO KUFUNGWA


 Mbunge wa Jimbo la Ilala Iddi Azan Zungu akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufika eneo la Jangwani lilolokumbwa na mafuriko na kusababisha barabara ya Morogoro kufungwa kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha leo Oktoba 26, 2017 Jijini Dar es salaam.
Kituo cha mabasi ya mwendo kasi cha Fire kikiwa kimesimama kutoa huduma kwa abiria baada kujaa maji kwa  bonde la Jangwani na kufunika barabara kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es salaam leo Oktoba 26, 2017.
Eneo la bonde la Jangwani likiwa limefurika na kuziba barabara ya Morogoro kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es Salaam.

 Barabara ya Morogoro ikiwa imefungwa kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es salaam.

Gari za mwendokasi zikiwa zimesitisha huduma kwa sasa kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha leo Oktoba 26, 2017 Jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment