Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, May 28, 2015

RC NJOMBE AWATAKA WAFANYABIASHARA WASIGOMBANE NA SERIKALI BADALA YAKE WAFANYE USHINDANI WA KIBIASHARA


 HUYU NI MKURUGENZI   UTAFITI  ,UTETEZI  WA USHINDANI  NA MIUNGANO YA KAMPUNI  TUME YA USHINDANI {FCC} BWANA ALLAN  MLULLA






 AFISA  MWANDAMIZI ,UTETEZI  WA USHINDANI BWANA  ALEX MMBAGA
 SOMO LIMEWAKOLEA WAFAYANYABIASHARA NJOMBE


 HAWA  NI WASHIRIKI WA SEMINA HIYO AMBAYO INAENDELEA SASA HIVI KATIKA UKUMBI WA FM HOTEL -NJOMBE


 MKURUGENZI   UTAFITI  ,UTETEZI  WA USHINDANI  NA MIUNGANO YA KAMPUNI  TUME YA USHINDANI {FCC} BWANA ALLAN  MLULLA  AKISOMA RISALA FUPI KWA MGENI RASMI

 MKUU WA MKOA WA NJOMBE BAADA YA KUWASILI KATIKA UKUMBI WA SEMINA LEO

 MFANYABIASHARA  PANGAMAWE  AKIWA NA MFANYABIASHARA MWENZAKE  BWANA CHAPWILA   WAKIJIANDAA KUHOJI MASWALI  KWENYE SEMINA HIYO BAADA YA HOTUBA YA MGENI RASMI

 WASHIRIKI WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA HOTUBA YA MGENI RASMI JUU YA USHINDANI  WA KIBIASHARA



MKUU WA MKOA WA NJOMBE DKT REHEMA NCHIMBI AKITOA HOTUBA YAKE  LEO KATIKA UKUMBI WA  FM -HOTEL  BAADA YA KUPOKEA RISALA FUPI


Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe  Dkt Rehema Nchimbi Amewataka Wafanyabiashara  Mkoani Njombe Kuepukana  Na Swala La Siasa Badala Yake  Wafanye Biashara  Kwa Umakini Na  Kwa Mahesabu Makali  Ili Kupata Faida  Pamoja Na Kuondoa Chuki Za Kugombana Na Serikali.

Akizungumza  Kwenye Semina Ya Siku Moja  Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Nchimbi Amesema Kuwa  Wafanyabiashara Hawataweza Kufanikiwa Endapo   Hawataihusisha Serikali Kwa Kuwa Serikali Inatunga   Na Kutafsili Sheria,  Kutatua Baadhi Ya Changamoto Zinazowakabili   Na Kutoa Vyombo Vya Kuwalinda  Wafanyabiashara Hao.

Amesema Kuwa Wafanyabiashara Hao Watafute Njia Ya Kutatua  Na Kujenga Mahusiano Mema  Na Siyo Kugombana Na Serikali   Na Kuweka Dhana Sahihi Ya Ushindani Wa Kibiashara  Kwani Njombe Siku Chache Zijazo Itakuwa Ndiyo Lango Kuu La Maendeleo  Kutokana Na Ongezeko La Wakazi  Watakaokuwepo Kwenye Machimbo Ya Liganga Na Mchuchuma.


Awali Akisoma Risala Kwa Mgeni Rasmi  Mkurugenzi  Utafiti  Wa Ushindani,Utetezi Wa Ushindani  Na Miungano Ya Kampuni  Ya Ushindani  FCC   Bwana Allan  Mlula  Amesema  Kuwa Tume ya Ushindani Ni Chombo Kinachosimamia Utendaji Wa Uchumi Wa Soko Kwa Nia Ya Kuhakikisha  Misingi Ya Ushindani Nalindwa Na Kusimamiwa Ipasavyo Ili Kuwepo na fursa sawa Za Uchumi Miongoni Mwa Wazalishaji, Wasambazaji Na Walaji  Ambao Ni watumiaji wa mwisho wa bidhaa na huduma mbalimbali.

Aidha  Bwana  Mlulla  Amesema Kuwa Semina Hiyo  Inalenga Kuwajenga Wote na kuongezea weledi wa namna ya kuboresha utendaji wa shughuli Zao kwa lengo la kuleta utendaji wa ufanisi na tija Katika uchumi wa Mkoa na Taifa Kwa Ujumla.


Kwa Upande Wake Washiriki Wa Semina Hiyo  Wakiwemo Wafanyabiashara Na Wataalamu Wa Halmashauri  Na Mkoa Wa Njombe  Wamehoji    Mambo Mbalimbali Ikiwemo  Uhalali Wa  Wafanyabiashara Za Usafirishaji  Kuandika Kwenye Tiketi Kwamba Gari Likiharibika   Kampuni Haita Husika Na Chochote Juu Ya Kuwasafirisha Ikiwa Wamelipa Nauli  Na Kusema Kuwa Haki Inakuwa Wapi Majibu Ambayo Yamejibiwa Na Mtoa Mada.

No comments:

Post a Comment