Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, May 27, 2015

RC NJOMBE AUNDA TUME YA WATU SITA KUCHUNGUZA WALIOHUSIKA KATIKA MAUAJI YA BASIL MWALONGO ALIYEUWAWA NA WATU WANAOSADIKIKA KUWA NI ASKALI POLISI





 Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Rehema Nchimbi ameunda tume huru ya watu sita kuchunguza tukio la mauaji ya Basil Mwalongo (24) anayedaiwa kuuawa na polisi wa doria usiku wa Jumanne wiki iliyopita katika klabu ya pombe ya Nyondo Mtaa wa Kambarage mjini hapa, na kujeruhi mwingine mmoja Fred Sanga.
Dk. Nchimbi alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa nje ya ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe alipokuwa mgeni rasmi katika kikao cha umoja wa wanawake wa CCM mkoani hapa kilichoenda sambamba na semina ya kujiunga na mfuko wa bima ya afya ya jamii (CHF).

Hatua inakuja baada ya waandishi wa habari kumtaka mkuu huyo wa mkoa kulizungumzia tukio hilo, kufuatia Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Franco Kibona  kwa muda wa wiki sasa kupata kigugumizi cha kulizungumzia tukio licha ya kufuatwa mara kwa mara na wahabari kutaka ufafanuzi.

Mkuu huyo wa mkoa, alisema ameunda tume hiyo ambayo itakuja na kiini cha tukio la mauaji hayo yanayodaiwa kutekelezwa polisi, ambayo yalisababisha wananchi wa Njombe kuandamana kupinga mauaji hayo na kusababisha vurugu hali iliyowalazimu polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya.

Pia Nchimbi alilaani mauaji hayo na kusema kuwa hayapaswi kujitokeza tena kwa kuwa yanavuruga amani,  pamoja na kulaani waliochochea maandamano kwenda katika hospitali ya kibena na hivyo kusababisha adha kwa wagonjwa.

“Tukio hili la mauji ninalilaani kwa kuwa limesababisha kuvurugika kwa amani na kero kwa wagonjwa katika hospitali yetu ya kibena lakini pia nalaani wanasiasa waliochochea wananchi kuandamana kwenda hospitalini sehemu ambayo wagonjwa wanapatiwa matibabu na wanahitaji utulivu,” alisema Dk. Nchimbi.

Alisema kamati aliyoiunda ina jumuisha viongozi wanne wa madhehebu ya dini, na kwamba anatarajia kumpelekea majibu hivi karibuni mara baada ya kumaliza uchunguzi wake ili kujua nini kiini cha tukio hilo la mauaji na kuruhi, ambalo limeacha sintofahamu kwa wakazi wa Njombe hasa kutokana na jeshi la polisi mkoani hapa kukaa kimya kwa kushindwa kulizingumzia hadi sasa.




No comments:

Post a Comment