Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, May 12, 2015

Kufukuzwa kazi wafanyakazi wa Ressedents Hotel ya kizimkazi zanzibar


Na Takdir Ali-Maelezo.  

Wafanyakazi 38 waliodai kuachishwa kazi katika hoteli ya Rezidensi iliopo Kizimkazi Wilaya ya kusini Unguja  wameiomba  Serikali ya Mapindyuzi Zanzibar kuingilia kati mgogoro wa kuachishwa kazi na Mmiliki wa Hoteli hiyo.
Wamesema wamesikitiswa na Uongozi wa Hoteli hiyo kuwaachisha kazi wafanyakazi bila kuwepo kwa sababu yoyote ya msingi jambo ambalo ni kinyume na Mikataba ya ajira waliokubaliana wakati wa uajiri.
Akizungumza na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) kiongozi wa Wafanyakazi hao Mary Laurence Frank amesema wakati wakiwa  katika likizo walipata barua za kuachishwa kazi bila ya kujua sababu za msingi.
Amefafanua kuwa mara baada ya kupata barua za kuachishwa kazi tarehe 4/5/2015 na kutakiwa kufanya makubaliano (cliarence)na Muajiri wao tarehe 8/5/2015 lakini cha  kusikitisha wamekwenda Hotelini hapo  kuanzia saa mbili hadi saa kumi na mbili bila kuonana na kiongozi yoyote wa Hoteli hiyo.
“Tulikwenda kufanya makubaliano (cliarence) ili watukabidhi mafao yetu ya kuvunja mkataba na sisi tuwape vifaa vyao lakini wlifunga milango na hawakuturuhusu kuingia ndani”Alisema Mary.
Amefafanua kuwa madai ya kuachishwa kazi kutokana na msimu mdogo wa biashara (low season) ni kinyume na makubaliano ya mikataba waliokubaliana  na alisema madai hayo hayana ukweli ndani yake.
Kwa upande wake Mohd Ali Abdallah,  ambae ni miongoni mwa waliochishwa kazi, alisema wamiliki wa Hoteli hiyo wamekuwa wakiwadhalilisha kwa kiasi kikubwa wafanyakazi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla ikiwemo kuwatolea maneno ya kashfa.
Amesema wanachohitaji ni kukaa pamoja na Uongozi wa Hoteli na kuwapatia haki zao za msingi kwa mujibu wa sheria na taratibu za Ajira ili haki iweze kufanyika na kuiomba serikali kuwabana zaidi Wawekezaji wenye tabia ya kuwadhalilisha wafanyakazi Wazalendo.
 
KWA HISAN YA JIACHIE BLOG

No comments:

Post a Comment