Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, April 26, 2015

DIWANI ANUSURIKA KUCHAPWA FIMBO NA MBUNGE,ALIWAZUIA WANANCHI KUSHIRIKI MAENDELEO.

            Huyu ndiye Diwani wa kata ya Luilo pia mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa Mh.Mathei Kongo aliyenusurika kuchapwa bakora kutokana na kupinga maendeleo

MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa katika Mkoa wa Njombe  Matei Kongo ambaye  ni diwani wa Kata ya Luilo jana alinusurika kuchapwa viboko mkutanoni na Mbunge wa jimbo Ludewa Deo Filikunjombe kutokana na Diwani huyo kutuhumiwa kuhamasisha wananchi kukataa kushiriki shughuli za maendeleo ikiwemo kusafisha na kuchimba mashimo kwa ajili ya umeme.

Filikunjombe alifikia hatua ya kumchapa diwani huyo fimbo kama angekuwepo kwenye mkutano kutokana na wananchi wa kata hiyo kumwambia kuwa diwani wao amekuwa akiwahamasisha kukataa kushiriki nguvukazi ya kuchimba mashimo kwa madai kuwa serikali ndiyo yenye jukumu hilo na kwamba kunafedha kwa ajili ya kazi hiyo siyo wananchi kuchimba.

‘’wananchi msinililie mimi jililieni wenyewe na diwani wenu ambaye anazuia maendeleo yenu,fedha hizi siyo za Halmashauri ya wilaya ya Ludewa nimezitafuta mimi, wananchi tukiiachia serikali pekeyake umeme huu hatuwezi kuupata mapema lakini tukichangia nguvu zetu umeme utawaka june mwaka huu yaani miezi miwili tu ijayo kiongozi anayekataa kuleta maendeleo ni mbya sana angekuwepo hapa ningemchapa fimbo mbele yenu bahati yake amekimbia.’’ alisisitiza Filikunjombe


Mwenyekiti wa kijiji cha Kipangala kilichop kata ya Luilo Jeremia Kayombo alikiri mkutanoni hapo kuwa Diwani wao alimpigia simu kuwa awaambie wananchi wasijitolee nguvu kazi kwa kuchimba mashimo kwa sababu hiyo syo kazi yao na kwamba hiyo ni kazi ya serikali, hata hivyo wananchi walikataa mawazio ya diwani huyo

Akiongea kwa hasira mmoja wa wananchi wa kijiji cha Luilo Bi.Stera Haule alidhibitisha kuwa Mh.Kongo alikuwa akipiga kampeni ya kuwahamasishi wananchi kutokushiriki katika kazi hiyo ya kimaendeleo baada ya Mbunge wa jimbo la Ludewa Mh.Deo Filikunjombe kufanya mikutano na wananchi na kuwahimiza kushirikiana na wataalamu wa umeme katika kuchimba mashimo hayo ili kuharakisha mradi huo kutekelezwa kwa muda mfupi.

Bi.Stera alisema wananchi wanachohitaji ni maendeleo na si siasa kwani kwa muda mrefu wamekuwa wakisubiri nishati hiyo ya umeme itapatikana lini lakini baadhi ya viongozi ambao ni tegemeo kwa chama cha mapinduzi wamekuwa wakikwamisha utekelezaji wa ilani ya chama hicho ambayo inataka kuleta maendeleo wa wananchi na Taifa kwa unjumla kwa muda mfupi.

Akitoa taarifa kwa mbunge Afisa mtendaji wa kata ya Luilo Daniel Henjewele kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Lifua alisema kuwa yeye alimtaarifu diwani wake kuhusu ziara ya mbunge lakini akamjibu kuwa anakwenda kuhudhuri kikao cha kamati ya mipango na fedha wilayani kwa sababu kina posho na yeye hana fedha ya kula.
 
‘’ mimi nilimtaarifu diwani wangu kuhusu ziara ya mheshimiwa mbunge lakini alisema hawezi kuhudhuria ziara ya mbunge kwa sababu anakwenda kwenye kikao cha kamati ya fedha na hana fedha ya kula, mimi sina kosa na wala sizuii maendeleo na mimi ni mtendaji ila anayezuia anafahamika hayupo hapa’’ alisema Henjewele

Kwa upande wake mkurugenzi wa uendeshaji katika kampuni ya power magic electrica contractor Aron makulu alisema kama wananchi watasubiri serikali na mkandarasi kufanyakazi zote mradi huu unawezakukamilika hapo mwakani lakini kama mpango wa mh, Filikunjombe utawezekana na wananchi kujitokeza kwa wingi mradi unaweza kukamilika baada ya miezi miwili tu.

Akizungumza kwa njia ya simu matei kongo alikana kuhamasisha wananchi kukataa kushiriki maendeleo kwa kusafisha njia na kuchimba mashimo kwa ajili ya nguzo lakini akakiri kuwaambia wananchi kuwa kazi ya kuleta  maendeleo ni jukumu la serikali na siyo wananchi kwa hiyo wananchi wanapaswa kulipwa. Hata hivyo wananchi wamepuuza kauli za diwani huyo na kuamua kwa kauli moja kushirikiana na mbunge wao kujiletea maendeleo.

Katika mradi huo vijiji 14 vya tarafa ya masasi vitanufaika ikiwemo Ngalawale, Kimelembe, Mkomang’ombe,Kipangala, Luilo,Lifua, Lihagule,Kingole,Igalu,Mbongo, Nsungu, Ilela,Ngelenge na Kipingu kama wananchi watajitokeza kwa wingi kupitia nguvukazi zao utakamilika ndani ya kipindi cha miezi miwili. @habari ludewa blog

No comments:

Post a Comment