Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, February 26, 2015

TASAF YAENDESHA SEMINA YA SIKU MBILI KWA WARATIBU WA MPANGO,WAHASIBU WA MPANGO,MAAFISA UFUATILIAJI, NA WAANDISHI WA HABARI KUTOKA MIKOA YA NJOMBE,MBEYA,IRINGA NA RUVUMA






MKURUGENZI  MTENDAJI WA  TASAF LADSLAUS   MWAMANGA AKIZUNGUMZA WAKATI WA UFUNGUZI





WAJUMBE WA KIKAO KAZI KILICHOFANYIKA MJINI NJOMBE











 Na Michael Ngilangwa

Mfuko Wa Maendeleo Ya Jamii (Tasaf) Umekiri  Kuwepo Kwa Vyombo Vya Habari Nchini Ndiyo Msaada Mkubwa Katika Kuhamasisha Mpango Wa Kunusuru Kaya Maskini Kwa Kutumia Kalamu Zao Kuelimisha Wananchi Juu Ya Mpango Huo.

Mkurugenzi Mtendaji Wa Mfuko Wa Maendeleo Ya Jamii (TASAF), Ladislaus Mwamanga Amesema Vyombo Vya Habari Ndiyo Vyenye Ushawishi Mkubwa Unaochangia Maendeleo  Ya Wananchi Waliowengi Wa Mijini Na Vijijini.

Akifungua Semina  Ya Siku Mbili Kwa Waratibu Wa Mpango, Wahasibu Wa Mpango, Maafisa Ufuatiliaji Na Waandishi Wa Habari Kutoka Mikoa Ya Mbeya, Njombe, Iringa Na Ruvuma,  Iliofanyika Katika Ukumbi Wa Kyando Mjini Njombe Mwamanga Amesema TASAF Hivi Sasa Imeona Iimalishe Mkakati Wa Mpango Kazi Kwa Ajili Ya Vyombo Vya Habari Ili Kuhabarisha Sifa Na Vigezo Vya Kaya Maskini.

Mwamanga Amesema Toka Wameanza Kutekeleza Mpango Huo, Umekwenda Vizuri Ambapo  Wamefikia Viwango Vya Kimataifa, Lakini Bado Kuna Dosari Kidogo Kwa Maana Uelewa Wa Watu Katika Ngazi Mbalimbali Bado Haujawa Mzuri Kwa Sababu Kuna Upotoshaji Wa Taarifa  Zinazohusu Mpango Huo.

Mkurugenzi Huyo Mtendaji Wa Tasaf Amesema Inawezekana Wapo Wananchi Wachache Hawajapata Taarifa Kuhusiana Na  Mpango Huo, Jambo Ambalo  Wameona Hivi Sasa Waimalishe Mpango Mkakati Wa Kupashana Habari Kwa Kutumia Vyombo Mbalimbali Ambavyo Vipo Katika Maeneo Ya Utekelezaji.

Amesema Kuwa Katika Kuanza  Ukurasa Mwingine Wa Kuboresha Ushirikiano Wanahabari Katika Maeneo Husika Na  Watendaji Katika Shughuli Za Mpango Wanapaswa Kuwa Kitu Kimoja, Pasipo Kutafutana Ubaya Katika Utendaji,  Badala Yake Wafanye Kazi Pamoja Kwa Kutumiza Malengo Ya Serikali.

Akizungumzia Umuhimu Wa Kutumia Waandishi Wa Habari Katika Mpango Wa Kunusuru Kaya Maskini Nchini, Amesema Ni Vyema Jamii Ikajitoa Kuwasaidia Wananchi Waliowengi.

Awali Akimkaribisha Mgeni Rasmi Mkurugenzi Wa  Kuwajengea Uwezo  Tasaf Bwana Fariji Mishael Amezuia Viongozi Wa Vijiji  Kuwekwa Kwenye Mpango Wa Tasaf Kuwa Kama Wanufaika Kwenye Mpango Kwani Wao Wanauwezo  Kupata Kipato Na Kuboresha Maisha Yao  Kuliko Walengwa Ambao Ni Kaya Masikini Huku Akisema Wanahitaji Kushauriana Kwa Kushirikiana Na Wanahabari Hivyo Ni Lazima Kusisitiza Hilo.

No comments:

Post a Comment