Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, February 25, 2015

MKUU WA MKOA WA NJOMBE AAGIZA HALMASHAURI KUTENGA MAENEO YA NYUMBA KWAAJILI YA WALIMU WANAPOSTAAFU

Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi Ameziagiza Halmashauri Zote Za Mkoa Wa Njombe  Kutenga Maeneo Ya Viwanja Kwaajili Ya Watumishi Wa Elimu  Hususani Walimu Ikiwa Ni Pamoja Na Kuwajengea Nyumba Ili Watakapo Staafu Waweze Kuwa Na Sehemu Za Kuishi.

Dkt Nchimbio Ametoa Agizo Hilo Wakati Wa Ufunguzi Wa Semina Ya Siku Sita Kwa Wakuu Wa Shule Za Sekondari Za Serikali Na  Za Watu Binafsi  Kinachofanyikia Katika Ukumbi Wa Turbo  Tangu Februari 23  Ambapo Semina Hiyo Imeandaliwa Na Watu Wa Ademu

Aidha Dkt Nchimbi Amesema Kuwa Ofisi Ya Mkoa Wa Njombe  Inatarajia Kuandaa Tuzo Kwa  Viongozi Wakuu  Katika Sekta Ya Elimu  Ambapo Amesema Hali Hiyo Itasaidia Kuwapa Motisha Na Moyo Wa Kufundisha  Na Kuondoa Manung'uniko  Miongoni Mwa Baadhi Ya  Wakuu Hao.

Katika Hatua Nyingine Dkt Nchimbi  Amewataka Wamiliki Wa Shule Za Watu Binafsi Kuwa Shirikisha Viongozi Wa Serikali Katika Kushirikiana Kutatua Baadhi Ya Changamoto Zinazowakabili  Huku Wakitakiwa Kuweka Mazingira Rafiki Kwa Watumishi Wao Na Wanafunzi  Ambayo Zoezi Hilo Linatakiwa Kufanywa Na Shule Zote Za Serikali Na Watu Binafsi.

Amesema Kuwa Mafunzo Yatakayo Tolewa Katika Semina Hiyo Wanatakiwa Kwenda Kuyatumia Vizuri   Na Kwenda Kusimamia Utekelezaji Wake  Wa Majukumu Huku Akisema Kuna Baadhi Ya Watendaji Wa Serikali Wamekuwa Kikwazo Kwa Walimu Na Kwamba  Wanatakiwa Kutoa Taarifa Kwa Viongozi Wa Ngazi Za Juu Kwa Wale Wanaowatishia Walimu Wakiwa Kazini.

Awali Akisoma Taarifa Fupi  Ya Mafunzo  Kwa Wakuu Wa Shule  Kuhusu Uongozi  Na Usimamizi  Wa Shule  Mkufunzi Kutoka Ademu Bi. Ester  Jonas Amesema Kuwa  Lengo La Mafunzo Hayo Ni   Kuwajengea Uwezo  Wakuu Wa Shule  Ili Kuimarisha Usimamizi Na Utendaji  Wa Elimu  Hususani Mpango Wa  Maendeleo  Ya Elimu  Ya Sekondari MMES 11.

Semina Hiyo Imewahusisha Wakuu Wa Shule Za Sekondari Kutoka Mkoa Wa Mbeya Na Njombe  Inatarajia Kuendeshwa Kwa Siku Sita Imedaiwa Itawasaidia Wakuu Wa Shule Hizo Kuboresha Kiwango Cha Taaluma Shuleni.

PICHA ZITAKUJIA HIVI PUNDE

No comments:

Post a Comment