Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, November 20, 2014

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI IRINGA ,LAJISALIMISHA POLISI


Gari la  Zimamoto mji Iringa  likiwa limesimama bila  kujua cha  kufanya baada ya  kufika  eneo la tukio ambalo walipigiwa  simu kuwa kuna moto unateketeza  nyumba ,taarifa za uongo
Askari  wa kikosi cha  Zimamoto na uokoaji Iringa wakitoka katika  nyumba iliyopo eneo la Zizi la Ng'ombe ambayo  walipokea taarifa  za  uongo kuwa nyumba  hiyo inawaka  moto
Askari  wa Zimamoto akitoka katika  nyumba ambayo ilidaiwa kuwaka  moto 
Askari  hao  wakijaribu  kupiga  namba ya  simu  iliyotumika  kutoa taarifa za  uongo juu ya moto
Hapa  askari  hao  wakijadiliana   
Hivi  ndivyo askari hao  walivyopoteza nguvu ya  kufanya kazi
Hapa wakijiandaa  kurudi  ofisini
Gari  likiwa katika spidi kali  kuwai kuzima moto  hewa
KIKOSI  cha  zima moto na uokoaji  katika Manispaa ya Iringa kimeamua  kufikisha malalamiko  yake kwa  jeshi la  polisi kufuatia mchezo mchafu unaofanywa na baadhi ya  watu  kupiga  simu za utoaji wa taarifa za uongozi  za  kuwepo kwa  moto hewa.

Akizungumza  leo mtandao huu wa matukiodaima.co.tz  mara  baada ya  kufika  eneo la Zizi la Ng'ombe  nje   kidogo ya  mji wa Iringa  kaimu  mkuu  wa kikosi cha Zima moto na uokoaji mjini Iringa Juma Joseph  alisema  kuwa  walipigiwa  simu  majira ya saa 5 asubuhi kuombwa  kufika  eneo  hilo kuwa  kuna nyumba inawaka  moto ila  baada ya  kufika hawakuweza  kuta  moto huo  wala mtu  aliyewapigia  simu.

" Kumekuwepo na mchezo  wa baadhi ya  wananchi  wa mji  wa Iringa  kupiga  simu ofisi za  Zimamoto kwa  lengo la  kutuchezea  akili  zetu na baadhi  wamekuwa  wakipiga  simu  ili  mradi  kusikia  sauti  zetu na kukata simu huku  wengine  wakitoa  taarifa  hewa za  moto"


Alisema  matukio kama  hayo  yameendelea  kuongezeka na kwa  hilo  tukio la Zizi la Ng'ombe  baada ya  kufika eneo hilo namba  iliyotumika  haikuweza  kupatikana na wenyeji  wa  eneo hilo kudai hakuna tukio la moto katika  nyumba   hiyo  waliyoelekezwa,


Hivyo  alisema  kutokana na  tukio  hilo wameona ni  vema  kwenda  polisi  ili kuikabidhi namba  hiyo  kwa ajili ya kumsaka  mhusika   huyo na kuchukulia hatua pamoja na kurudisha  gharama  za mafuta ambayo gari  hilo limetumia .


Alisema   mbali ya  kutumia mafuta ya  gari hilo pia jumla ya  pikipiki  mbili  za askari  wa  zimamoto  zilitumika  kwenda  eneo la  tukio  haraka  zaidi  ili  kufanya  shughuli ya uokoaji ila hakukuwa na moto  wowote.

Kiongozi   huyo aliwaonya  wananchi  wa mji  wa Iringa  kuepuka  kupiga simu za  kuwatania Zima moto  kwani  wakati mwingine mwenye  mchezo huo anaweza  kuwa na tatizo  kweli na  moto na  zimamoto  wakajua ni utani wa  siku  zote

No comments:

Post a Comment