Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, April 11, 2014

SHIRIKA LA SHIPO LATAMBULISHA MRADI WA SHULE YA CHEKECHEA JOSHONI NJOMBE


Southern Highlands Participatory Organisation

 

 
 WANANCHI WA MTAA WA JOSHONI WAKIWA KATIKA MAKUNDI YA MAJADILIANO KATIKA OFISI YA MTAA HUO

 DIWANI WA KATA YA MJIMWEMA AKIWAELEKEZA WANANCHI NA KUWAPANGA KATIKA MAKUNDI KUJADILI MRADI HUO WA UJENZI  WA CHEKECHEA HIYO

Na Erasto Mgeni Njombe

 Katika Kuhakikisha Miradi Mbalimbali Inatekelezwa Kupitia Asasi Zisizo za Kiserikali Mkoani Njombe,Mashirika Hayo Yameonekana Kuongeza Kasi Ya Kutekeleza Miradi Yao Kama Wajibu Wao Kwa Kushirikiana na Serikali.


Aidha Shirika Lisilo la Kiserika la SHIPO Lililopo Mkoani Njombe Hii Leo Limetambulisha Rasmi Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Chekechea Ambao Unatarajiwa Kujengwa Katika Mtaa wa Joshoni Kwa Kushirikiana na Wananchi wa Mtaa Huo.

Akitambulisha Mradi wa Ujenzi Huo Katika Ofisi za Mtaa wa Joshoni Mjini Njombe Mmoja wa Viongozi Kutoka SHIPO Bonaventura Mdamu Amesema Mradi Huo wa Ujenzi  Utahusisha Vyumba Viwili Vya Madarasa na Ofisi za Walimu .

Bwana Mdamu Ameongeza Kuwa SHIPO Ilikuwa na Mpango wa Ujenzi wa Shule ya Awali Katika Mtaa Huo Tangu Mwaka 2011 Huku Akiwaomba Wakazi wa Mtaa Huo Kutoa Ushirikiano Ili Kukamilisha Haraka Mradi Huo.

Jimmy Ngumbuke ni Diwani wa Kata ya Mjimwema Mjini Njombe Ambaye Amelishukuru Shirika Hilo na Kuuhakikishia Uongozi wa SHIPO Kuwa Wakazi wa Mtaa Huo Watashiriki Katika Mradi Huo Hadi Hapo Utakapokakamilika , Huku Afisa

Mtendaji wa Mtaa wa Joshoni Isabela Malangalila Akiuomba Uonngozi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe Kutoa Ushirikiano wa Miradi Inayotkelezwa Katika Mtaa Huo.

Shirika la SHIPO Limekuwa Likichangia Maendeleo Katika Sekta Mbalimbali Mkoani Njombe Hususani Katika Huduma za Kijamii.

No comments:

Post a Comment