Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, June 23, 2013

ASKARI POLISI IRINGA ALICHAFUA JESHI LA POLISI AFANYA KITENDO CHA UNYAMA KWA MKEWE ATOWEKA ...........

chanzo Francis  Godwin blog

 Hapa Rehema  akiwa  wodini katika  Hospital ya  Rufaa ya  mkoa  wa Iringa alipokimbizwa kwa matibabu kutokana na  kipigo kikali  toka kwa askari huyo
 Hapa  akionekana  mwenye uzembe  zaidi
 Hapa  akionyesha majeraha ambayo aliyapata  shingoni kutokana na kukabwa  shingo na askari huyo
 Hapa akiwa  hoi kwa  kipigo
 Bi Rehema Shauri  Madongo mkazi  wa  Wilolesi mjini Iringa akiwa na mtoto  wake  baada ya  kuponea katika  tundu la  sindano  kuuwawa kwa  kipigo kutoka kwa mmewe ambaye ni askari polisi mjini Iringa  kiasi cha  kukimbia nyumba na kurudi kwa  wazazi  wake
 stepen kanyala akiwa na mke  wake siku ya harusi yao iliyodumu kwa miaka  mitatu  sasa
 Bi  Rehema  akiwa nyumbani kwa  wazazi  wake  baada ya  kukimbia nyumba yake  kutokana na kipigo kisichokwisha
Mama  mzazi  wa  Rehema  akiwa Monica Shauri
IGP Mwema

WAKATI  jeshi la  polisi nchini likiendelea  kujiweka karibu na Raia  hata  kuamua  kuanzisha  dawati la jinsia  katika vituo  vya  polisi ,kwa  mkoa  wa Iringa baadhi ya askari  wanadaiwa  kupingana na jitihada  hizo za  polisi kwa  kushindwa  kuheshimu dawati  hilo na badala yake  kushiriki  kulivunjia heshima jeshi  hilo kutokana na kufanya  vitendo ambavyo ni kinyume na mkakati  wa jeshi hilo katika kuanzisha dawa.ti la jinsia.

Uchunguzi wa mtandao  huu wa www.matukiodaima.com na www.francisgodwin.blogspot.com umeonyesha  kuwa  dawati hilo kwa  askari  limekosa  kuheshimika kutokana na vitendo vya unyanyasaji  wa kijinsia ambavyo  baadhi ya askari  (30) wamekuwa  wakifanya kwa watoto  wao na  wake  zao.

Rehema Shauri Madongo  ni  mmoja kati ya  mwanamke ambaye amebahatika kuolewa na askari polisi kitendo  cha upelelezi ambaye anaeleza  jinsi alivyotendewa  vitendo  vya ukatili wa kijinsia kwa  kuteswa na  kupigwa kikatili  na pindi anapofika  polisi hakuna hatua  zozote  zinazochukuliwa kwa mtuhumiwa huyo ambaye ni askari .
" Mimi  niliolewa kwa  ndoa na Stephen Kanyala  ambae ni askari  kitengo cha upelelezi ila  baada ya  kuolewa  ukiwa umepita  mwezi  mmoja  tuo nilianza  kushuhudia  mateso ya  ndoa kutokana  na kipigo  na mateso makali  niliyokuwa  nikiyapata"
Anasema  kuwa kila  wakati pindi anapotaka  kujua  jambo  kutokana kwa mume  wake  huyo hasa pale anapoona jumbe  zenye  utata katika  simu  yake ambazo  zimetoka kwa  wanawake anaiowatambua  vizuri amekuwa akijibiwa kwa  kipigo kikali.
Rehema alisema  kuwa ni  rahisi kwake  kuweza  kuhesabia siku ambazo hajapigwa kuliko  kuhesabi siku ambazo amepigwa ambazo ni nyigi  zaidi .
Kwa  alisema toka  ameolewa  kila  mara  amekuwa akipokea  kipigo na mbaya  zaidi kabla ya  kupigwa amekuwa akifungwa  mikono kwa  pingu zinazotumika  kuwafunga  watuhumiwa pingu ambazo mume  wake  huyo amekuwa akizihifadhi  ndani ya  nyumba  .
" Kweli inasikitisha  sana kusimulia kwani kabla ya  kupigwa  nimekuwa  nikifungwa  pingu mikono kama mharifu sugu na baada ya hapo  kipigo  kikali kimekuwa kikinikuta ....hadi  sasa  nimepigwa  zaidi ya  mara  20 na polisi  nimekwenda  kuripoti mara  tatu na Hospital nimelazwa mara moja ila  siku nyingine  nimekuwa nikiugulia nyumbani ila nyumbani kwa  wazazi  nimerudi mara tatu sasa"
Alisema   kuwa mbali ya  kupigwa na  kuumizwa  ila  kuna mateso mengine ambayo amekuwa akiyapata  kutoka kwa  mwanaume  huyo ni siri yake na hayapaswi kuelezwa hapa kutokana na jinsi ambavyo askari  huyo anavyomtenda ukatili  wa kinyama.
Hata  hivyo  alisema kuwa akiwa na mimba ya mwezi mmoja hali ya  kipigo ilizidi  zaidi na wakati mwingine  alipata  kumfunga  shingo na kanga  kwa  kutaka kunyonga shingo  huku akitishi  kumuua .
Alisema  kuwa baada ya  kujifungua mtoto  wa njia ya Oparesheni mwanaume huyo alimpiga  kiasi cha kumjeruhi mtoto  wa mwezi  mmoja kwa  kumpiga kofi ambalo  lilielekezwa  kwake na bahati mbaya  likaishia kwa mtoto.
Aidha alisema  kuwa kila akifika  polisi  kufungua kesi hakuna utekelezaji  unaofanyika kutokana na polisi  kulindana na  kuwa suala  hilo la askari  polisi  kulindani  lilianza toka wakati kamanda wa  polisi akiwa Evarist Mangala ,pia alipofika kamanda Michael Kamuhanda  ambaye kwa  sasa amehamishwa baada ya  cheo kupanda  pia amepata  kufikisha malalamiko yake  ila hakuna  jipya ila  sasa amefikisha  tena  suala  hilo kwa kamanda mpya RPC Ramadhan  Mungi ambae amedai  kuwa na imani  nae  zaidi katika  kulishughulikia  suala lake

Pia  alisema mbali ya  kupigwa akiwa  nyumbani kwake  ila bado anapoamua kukimbia nyumba  hiyo  na  kukimbilia kwa  wazazi  wake  bado askari  huyo amekuwa akimfuata na kumpa  kipigo mbele ya  wazazi  wake .

Hivyo alisema  katika  kunusuru uhai  wake kwa  sasa ameamua  kurudi kwa  wazazi  wake na suala la ndoa hataki  tena .
 Kwa  upande  wake Mama  mzazi  wa  Rehema  akiwa Monica Shauri alisema  kuwa amechoka  kuuguza  binti yake kwa  kipigo na  kuwa kuna  wakati mwanaume  huyo amekuwa akitishia  kumpiga hata  yeye.
Hivyo alisema  kwa  sasa mbali ya kumtoa binti yake Hospital ila wamekuwa wakiishi ndani  wamejifungia milango kuogopa askari  huyo  kuja kuwafanyia ukatili ikiwa ni pamoja na kuwaua kwa risasi kama ambavyo amekuwa akiwatisha mara kwa mara  kuwa dawa yao inachemka na ipo  siku  wataonja mauti.
Bi Shauri alisema mbali ya kuwa yeye ni mmoja wa wacha Mungu kwa maana na Mlokole mzuri ambae kila  wakati asubuhi lazima aende  kusali ila kwa sasa anaogopa kutoka asubuhi kwa kuhofia kuvamiwa na askari  huyo .
Hivyo aliomba jeshi la  polisi  kuweza kumpa ulinzi yeye na familia  yake ama kumkamata mtuhumiwa  huyo ambae inadaiwa kwa  sasa yupo katika mji wa Iringa ila askari  wenzake  wanamlinda.
Kuhusu uamuzi wa  binti yake wa kuomba ndoa hiyo kuvunjwa alisema anaungana na binti yake  kuikataa ndoa hiyo na kuwa kwa  sasa  wapo tayari  kurudisha mahali yake ya Tsh 200,000 ambazo  alizitoa kama mahali ili kunusuru uhai wao na uhai wa mtoto  wake  huyo.

No comments:

Post a Comment