Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, March 3, 2018

MUNGU AILAZE MAHALA PEMA ROHO YA MAREHEMU ASKOFU WA KANISA LA CALVARY NJOMBE NA IRINGA NA MTUME JOHN BAZORO.AMEN

 ASKOFU MKUU  WA CALVARY   DAUSIDAU HAULE MABOYA  AKIHUBIRI  KATIKA MSIBA  WA ASKOFU  WA  JIMBO LA NJOMBE  NA  IRINGA
 MKUU  WA MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA  OLE  SENDEKA  AKIWA  KWENYE  MAZISHI  YA  ASKOFU JOHN BAZORO WA CALVARY NJOMBE  NA  IRINGA.





NJOMBE

Askofu  Wa Kanisa  La  Calvary  Jimbo  La  Njombe  Na  Iringa    Mtume  John  Bazoro   Amefariki  Dunia  February  24  Wakati  Akipatiwa  Matibabu  Katika  Hospitali  Ya  Makikaliuki  Jijini  Dar Es  Salaam  Na  Mwili  Unatarajia  Kusafirishwa  Siku  Ya  Kesho February  27.

Makamu  Askofu   Wa  Kanisa  La  Kalvary   Jimbo  La  Njombe  Na  Iringa  Mch. Peace  Kameta  Amesema   Mwili Wa  Marehemu Askofu  Mtume  John  Bazoro  Unatarajia  Kuzikwa  Katika  Kanisa  La  Kalvary  Lililopo  Mtaa  Wa  Block  X  Nyuma  Ya  Uwanja  Wa  Ndege  Njombe  Mjini.

Makamu  Askofu  Kameta  Amesema  Marehemu  Amelitumikia  Jimbo  Hilo  Kwa  Uaminifu  Na  Ukaribu  Zaidi  Na  Kutaka  Waumini  Wa  Kanisa  Hilo  Kuwa  Wavumilivu  Katika  Kipindi  Hiki  Kigumu  Cha  Kuhami  Msiba  Wa  Askofu  Wao  Wa  Kanisa  La  Kalvary.

Amesema  Marehemu  Atakumbukwa  Kwa  Mengi Aliyoyafanya  Enzi  Ya  Uhai  Wake  Kwani   Ameacha  Zaidi  Ya  Makanisa  25  Ambayo  Yamefunguliwa  Na  Yanaendelea  Kutumika  Katika  Jimbo  La  Iringa  Na  Njombe.


Baadhi  Ya  Waumini  Wa  Kanisa  La  Kalvary  Njombe  Mjini   Wamemuelezea  Marehemu  Askofu  Na  Mtume  Bazoro  Namna  Alivyowatumikia   Waumini  Wake  Kwamba  Alikuwa  Karibu  Nao  Na  Alitoa  Huduma  Kwa  Ukaribu  Zaidi  Lakini  Wao  Walimpenda  Ila  Mungu   Amempenda  Zaidi.


Mazishi  Ya  Askofu  Wa  Kanisa  La  Kalvary   Jimbo  La  Njombe  Na  Iringa  Yanatarajiwa  Kufanyika  Kesho  Katika  Kanisa  La  Kalvary  Mjini  Njombe.

Bwana  Ametoa   Na  Bwana  Ametwaa   Jina  La  Bwana  Libarikiwe.
......................

No comments:

Post a Comment