Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, February 14, 2018

WABUNGE CCM WAMIMINIKA KUMUOMBEA KURA MTULIA UBUNGE JIMBO LA KINONDONI


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kupitia viongozi wake wa ngazi mbalimbali wameendelea kunadi sera za maendeleo na kumuombea kura mgombea wao wa ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam huku baadhi yao wakisema uchaguzi huo ni sawa na usajili wa dirisha dogo.

Hivyo wanatumia usajili huo kwa ajili ya kumpata Mtulia ambaye wanaamini ni mtu sahihi kwa maendeleo ya wananchi wa Kinondoni kwani alikokuwa awali hakuwa nafasi ya kushirikiana na Serikali ya Rais ,Dk.John Magufuli kufanya maendeleo.

Wakizungumza kwenye kampeni za uchaguzi huo unaotarajia kufanyika Februari 17(Jumamosi ya wiki hii), viongozi wa CCM wakiwamo baadhi ya mawaziri ambao wamefika kwenye kampeni hizo kwa nafasi zao za ubunge,wamewaambia wananchi hao Mtulia ndio mtu sahihi kwao.

Mgeni rasmi kwenye kampeni zilizofanyika leo Kata ya Ndugumbi ambaye pia ni mbunge wa Mbinga Sixtus Mapunda amesema anatambua uwezo wa Mtulia na hivyo ni vema wananchi wakamchagua ili awatumikie kikamilifu.

Amewaeleza wananchi kuwa uchaguzi mkuu ulishafanyika mwaka 2015 na sasa ni uchaguzi mdogo ,hivyo Chama ambacho kimepewa dhamana ya kuongoza ni CCM na kwa maana hiyo Mtulia akiwa mbunge atashirikiana na viongozi wengine kuleta maendeleo ya wananchi.
 

Amefafanua anaufananisha uchaguzi huo na usajili wa dirisha dogo ambapo tayari CCM wanayo timu nzuri yenye ushindani wa hali ya juu na iliyokuwa na ari ya kuwatumikia wananchi,hivyo kwenye usajili huo wanamtaka Mtulia kuboresha timu yao.

 "CCM ni timu ambayo inawachezaji wazuri na waliotumia kwenye kila idara na kama mnavyojua kwenye usajili mdogo lazima msajili mchezaji ambaye atakuwa na uwezo na anaendana na kasi na timu ambayo tunayo.Hivyo Mtulia ni mtu sahihi kwetu.

"Kule alikokuwa mwanzoni hakuwa na uwezo wa kufanya maendeleo kwani kila akitaka kufanya wenzake wanamzuia kwa kigezo kuwa yakipatikana maendeleo ya Kinondoni upinzani hautakuwa na nafasi mwaka 2020.Hivyi akiwa CCM atafanya maendeleo kwa kasi kubwa na tutampa ushirikiano kadri ya uwezo wetu,"amesema Mapunda.

No comments:

Post a Comment