Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Wednesday, February 21, 2018

MKUU WA MKOA WA NJOMBE CHRISTOPHA OLE SENDEKA AMEAGIZA KUSIMAMISHWA NA HALMASHAURI YA MJI WA NJOMBE KUVUNJA MKATABA NA KAMPUNI YA IHAGALA AUCTION MART


 
 MKUU WA MKOA  WA  NJOMBE  CHRISTOPHA OLE SENDEKA  AKITOA  MAAGIZO KWA  HALMASHAURI YA MJI  WA  NJOMBE KUVUNJA  MKATABA  NA  KAMPUNI YA IHAGALA AUCTION MART  KUTOKANA  NA  KUINGIZWA KATIKA  KAZI  YA KUKUSANYA  MAPATO BILA  TARATIBU ZA  MANUNUZI  KUFUATWA, KUTANGAZA  ZABUNI  HAZIKUTANGAZWA  NA UNYANYASAJI  KWA WANANCHI NI MKUBWA  UNAOFANYWA  NA KAMPUNI HIYO.
 
 VIONGOZI  WA  JUMUIYA  YA  WAFANYABIASHARA  WA NJOMBE  WAKIWA  NA MKURUGENZI  WA  HALMASHAURI YA MJI  WA  NJOMBE  PAMOJA  NA MKUU  WA  WILAYA  NA  VIONGOZI  WENGINE  WA  CCM KWENYE MKUTANO  WA  WAFANYABIASHARA  NJOMBE  MJINI.




 WAFANYABIASHARA  WAKIWA  KWENYE  UKUMBI  WA  TURBO  KUTOA  KERO  ZAO  DHIDI  YA MSANGU.

 MKURUGENZI  WA  KAMPUNI  YA  IHAGALA  AUTION MART  INAYOMILIKIWA  NA  CAROS  MSANGU  AKIJIBIA  BAADHI  YA  HOJA  ZINAZOMUHUSU  YEYE  NA  KWANINI  ANATUMIA  GARI  LA  SERIKALI  KWA  KAZI  ZAKE  BINAFSI.




MWANASHERIA  WA  HALMASHAURI  AKIWA  NA  MKURUGENZI  WA  IHAGALA  AUCTION MART  WAKISAIDIANA  KUJIBU HOJA  ZINAZOULIZWA  NA  WAFANYABIASHARA  ZILIZOELEKEZWA  KWA  MKUU WA  MKOA  WA  NJOMBE.

Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Christopha  Ole Sendeka  Ameagiza Kusimamishwa  Kampuni  Ya Ihagala  Auction  Mart  Inayosimamiwa  Na  Caros  Msangu  Kutokana Na  Kukiukwa  Kwa  Sheria Ya  Manunuzi  Na Kuagiza  Kuvunjwa  Kwa  Mkataba  Wake Na  Halmashauri  Ya Mji  Wa  Njombe  .

Hatua  Hiyo  Ya  Mkuu  Wa  Mkoa  Wa  Njombe  Ole Sendeka  Ya  Kuisimamisha  Kampuni  Ya  Ihagala  Auction Mart   Imetokana  Na  Malalamiko  Ya  Wafanyabiashara  Kulalamikia   Kampuni  Hiyo  Kutumia  Mamlaka  Vibaya   Huku  Wakisema  Upatikanaji  Wake  Haukufuata  Sheria  Ya  Kutangaza  Zabuni.

Bwana  Sendeka  Amesema  Kampuni  Hiyo  Imeonekana  Kufanya  Kazi  Ya  Kukusanya Mapato  YHalmashauri  Kwaajili   Ya  Viongozi  Fulani  ,Kutumia  Gari  La  Serikali, Kuwakejeli  Wafanyabiashara  Ambapo  Hata  Alipotaka  Kupewa  Ufafanuzi  Namna  Ilivyopatikana  Imeonesha  Alikwenda  Kiundugu.

Akijibu  Maswali  Ya  Mkuu Wa  Mkoa Wa  Njombe ,Mkurugenzi  Wa  Kampuni  Ya  Ihagala  Auction Mart  Caros  Msangu  Amesema  Yeye  Anafanya Kazi  Kwa  Mujibu  Wa  Sheria  Kwani  Ana Mkataba  Na  Halmashauri  Ya  Mji  Wa  Njombe  Wa  Kukusanya  Mapato  .


Awali  Wafanyabiashara  Wamefikisha  Kero  Mbalimbali  Kwa  Mkuu  Wa Mkoa  Wa  Njombe  Christopha  Ole  Sendeka  Kwamba  Gari  La  Serikali  Linatumiwa  Na  Kampuni  Binafsi, Ukamataji  Usiyo  Na  Staha,  Uwepo  Wa  Tozo  Zinazoashiria  Kuomba  Rushwa  Huku  Mwenyekiti  Wa  Jumuiya  Ya  Wafanyabiashara JWT  Onesmo  Mwajombe  Akishukuru  Kwa Maamuzi  Hayo  Ya  Kuisimamisha  Kampuni  Hiyo.

Aidha  Wafanyabiashara  Hao  Wamesema  Kuwa  Baadhi  Ya  Michango  Hawana  Imani  Nayo  Kwani  Baadhi  Ya  Fedha  Zinaishia  Kwenye  Mifuko  Ya  Kampuni  Hiyo   Ambayo  Mkurugenzi  Na Watalaamu  Wa  Halmashauri   Ya  Mji  Wa  Njombe  Wameshindwa  Kutolea  Majibu  Yakumuridhisha  Mkuu  Wa  Mkoa.

Hivi  Karibuni  Kikao  Cha  Baraza  La  Madiwani Wa  Halmashauri  Ya  Mji  Wa  Njombe  Kiliwasimamisha  Madiwani  Watatu  Akiwemo  Diwani  Wa  Viti  Maalumu  Tarafa  Ya  Njombe  Mjini Sekrada  Mligo,  Diwani  Wa  Kata  Ya   Ramadhani  Geoge  Sanga  Na  Diwani  Wa  Kata  Ya  Iwungiro  Bwana  Danda  Ambao  Walionekana  Kushikilia  Shilingi  Ya  Kutaka  Ijadiliwe  Hoja  Ya Uwepo Wa Msangu  Na Kusimamishwa  Vikao  Vitatu.



No comments:

Post a Comment