Katika Kikao hicho Bodi ya Korosho Kupitia MAMCU walisema, wameagiza magunia Million1 kupitia Kampuni ya DIRMAN HOLDING LTD na Ndipo mkuu wa Mkoa akaagiza Kuletewa mkataba Huo na kubaini kuwa Baadhi ya wajumbe wa Mamcu Hawaujui Mkataba na Haujulikani Thamani yake laki pia Mkataba ni magunia Laki6.5 na sio Million1 walizozisema katika kikao Hicho.Hata hivyo magunia hayo mpaka sasa hayajulikani idadi kamili iliyoletwa
Katika Mkutano na waandishi wa Habari Ofini kwake, Mkuu wa mkoa Byakanwa amesema kutokana na Udanganyifu huo Ofisi yake imeamua Bodi ya Korosho isilipe Pesa yeyote kwa kampuni ya DIRMA HOLDING LTD kwa kushindwa kuleta magunia kwa wakati,kwani ilitakiwa kuleta Septemba 30/2017lakini mpaka sasa bado hajakamilisha na hakuna hatua zozote zilizochukuliwa dhidi ya Mzabuni huyo.
Aidha Ameiagiza Bodi kuhakikisha inasambaza magunia ndani ya Kipindi cha Wiki Mbili zijazo ili malalamiko ya wakulima yaweze kuondoka.
Kutokana na Udanganyifu Huo Mkuu wa Mkoa anatarajia Kuunda kamati ili kuweza kuchunguza taratibu zinazotumika kuingia mikataba na wote waliohusika na kamati hiyo itaishauri nini cha kufanya kwa wahusika.

No comments:
Post a Comment