Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, November 5, 2017

MUYAHUDI AMWAGA MAMILIONI YA PESA UTENGULE MAKAMBAKO, NI ZAIDI YA MILIONI 50




 MWENYEKITI  WA HALMASHAURI  YA  MJI  WA MAKAMBAKO  HANANA  MFIKWA  AKITETA JAMBO  NA MFADHILI  HUYO BWANA ISDORY L.MWELADZI MAARUFU KAMA MUYAHUDI  BAADA YA KUWASILI MEZA KUU.
 
 MTENDAJI  KATA  YA  UTENGULE  JOB LUPONELO  FUTE  AKISOMA  RISALA  FUPI  YA MGENI RASMI  AKIWA  NA  AFISA  ELIMU KATA  YA UTENGULE.
 
 DIWANI  WA KATA  YA  UTENGULE  STEPHAN  MGOBA  AKITOA  NENO LAKE  LA  SHUKRANI KWA MAMBO  WALIOSAIDIWA  NA  BWANA  MWELADZI.
 

 MUYAHUDI  AKINONG'ONEZWA  JAMBO  LA  MZEE MWENZAKE  HAPA WANANG'ATANA SIKIO.
 MWENYEKIJI  WA  KIJIJI  CHA  UTENGULE  AKIFUNGUA  MKUTANO  ULIYOFANYIKA  JANA  KATIKA KIJIJI  CHAKE  CHA  UTENGULE.
 
 HITRA  BENJAMINI  MSOLA  KATIBU   WA  ITIKADI  NA  UENEZI  WILAYA  YA  NJOMBE  AKIZUNGUMZA MBELE  YA  MKUTANO HUO  WA  UTENGULE.



 BAADHI YA WADAU  AMBAO  NI  WANANCHI  WA  UTENGULE  WAKITETA  JAMBO HAPA KWA FRAHA KUBWA.


WAZEE HAWA  NAO  WALIFIKA  KUSHUHUDIA  UTOLEWAJI  WA PESA  KUTOKA  KWA  MWANANCHI  MWENZAO  ISDORY  MWELADZI MAARUFU KAMA MUYAHUDI  WAKO  PEMBENI KABISA  NA  KUNDI  LA  WANANCHI  WALIOKUSANYIKA.


MWENYEKITI  WA  HALMASHAURI YA  MJI   WA  MAKAMBAKO  HANANA  MFIKWA  AKIZUNGUMZA  BAADA  YA  KUTOA  AKAUNTI  ZA  BENKI ZA  VIJIJI KWAMBA  MDAU  HUYO  AMESAIDIA  SERIKALI  PALE  AMBAPO  HALMASHAURI ILITAKIWA  KUCHANGIA  SASA  AMESAOIDIA YEYE  NA KUOMBA  NA WADAU WENGINE  KUIGA MFANO HUO.



HUYU  NI  KAKA  YAKE  NA  MFADHILI  MUYAHUDI  ANAFAHAMIKA  KWA  JINA  LA MWALIMU  ANJAWE  L. MWELADZI  MAARUFU KAMA MKALI  AKIZUNGUMZA NA KUTOA NASAHA  ZAKE.




WAKAZI   WA  KATA   HII  PIA  NI  WAJASILIAMALI WANAJISHUGHULISHA NA KILIMO CHA  MBOGAMBOGA  KAMA UNAVYOONA.




FRAHA  IOJE  KWA  HAWA  WAKAZI   WA  KATA  HII TAZAMA  BURUDANI HII


 
ANAITWA  JENIFER  AMBAYE  YUKO KATIKA  SHULE  YA MSINGI UTENGULE  NAYE  KWA FRAHA ANAWAPIGIA  GITAA


























 ALIYESIMAMA  NA FIMBO NI DADA  YAKE  NA MFADHILI  HUYO BWANA MUYAHUDI



































NJOMBE

Zaidi Ya  Shilingi  Milioni  Hamsini   Zinatarajiwa  Kuingizwa  Kwenye  Akaunti Za Benki  Za  Vijiji  Vya  Kata  Ya  Utengule  Kuanzia  Alhamishi  Wiki  Hii  Kwaajili   Ya  Kuanza  Utekelezaji   Wa  Miradi  Mbalimbali  Ikiwemo  Zahanati  Na  Miradi  Ya  Maji.

Hayo  Yamesemwa  Na  Mdau   Wa  Maendeleo  Wa  Kata  Ya  Utengule Isdory  Mweladzi  Maarufu  Kama  Muyahudi   Mbele  Ya  Uongozi  Wa  Halmashauri  Ya  Wilaya  Ya  Njombe  Ukiongozwa Na Mwenyekiti  Wa   Halmashauri Ya Mji Makambako  Katika  Siku Ya Kukabidhiwa  Fedha Zilizoahidiwa  Mwezi  Mmoja  Uliopita.

Bwana  Mweladzi  Amesema  Pamoja  Na  Changamoto  Mbalimbali  Ambazo  Zimekuwa  Zikijitokeza  Kwa Wananchi   Amelazimika  Kurudi   Nyumbani  Kwake  Ambako  Ni Kata  Ya  Utengule  Kusaidiana  Na  Wananchi Katika  Shida  Na  Raha  Huku  Akiomba Na Wadau  Wengine  Wa Maendeleo  Kujitokeza  Kusaidia  Baadhi  Ya  Miradi   Katika  Kata  Hiyo.

Bwana  Mweladzi   Amekemea  Pia Tabia  Za  Baadhi  Ya  Viongozi  Kutumia  Fedha  Za  Serikali  Na  Zile Zinazotolewa  Na  Wafadhili  Kutumia  Kwa  Maslahi Yao  Binafsi  Kwamba  Asiwepo  Mtu  Wa Aina Hiyo   Kwani  Iwe  Kanisani, Maofisini  Fedha  Zinakuwa  Haziko  Salaama.


Muyahudi Amesema  Bado Atasaidia  Pia  Kukarabati  Tenk  La  Maji   La  Kijiji  Cha  Utengule Ili  Wananchi  Wa Kata Hiyo  Waepukane  Na  Changamoto Ya  Kukosekana  Kwa  Maji  Huku  Zahanati  Ya Kijiji Cha  Utengule  Ambako  Amezaliwa  Na  Kusoma  Hapo  Akiahidi  Kuiezeka  Mwenyewe Ili  Michango  Ipunguzwe  Kwa  Wananchi.

Mwenyekiti  Wa  Halmashauri  Ya  Mji  Wa  Makambako  Hanana  Mfikwa  Amepongeza  Kwa  Juhudi  Na  Moyo  Aliyonao  Mfadhili  Huyo    Kwa  Msaada  Wake  Huku  Akiwataka  Viongozi  Wa  Kata  Hiyo  Kuanza  Mchakato   Wa  Manunuzi  Ili  Miradi  Ianze Kutekelezwa  Kwa  Haraka  Na Kuhakikisha  Fedha  Hizo  Zinafanya  Kazi  Iliyokusudiwa.

Afisa  Mtendaji  Wa  Kata  Ya  Utengule  Job Fute  Akisoma  Taarifa Ya  Kata  Ameshukuru  Mfadhili  Huyo  Kwa  Kutoa  Misaada  Mbalimbali Ikiwemo  Kusaidia  Ujenzi  Wa Zahanati,Ofisi,Shule Na Kanisa  Huku  Diwani  Wa  Kata  Hiyo  Stephano  Mgoba  Akiahidi  Ushirikiano  Mkubwa Kusimamia Maendeleo Ya  Vijiji  Na  Kata.

Mdau  Huyo  Wa  Maendeleo  Bwana  Mweladzi  Maarufu  Kwa Jina  La  Muyahudi   Tangu  Mwanzo  Ameonekana  Kusifika  Kwa  Kusaidia  Shughuli   Mbalimbali   Katika  Kata  Hiyo   Ambayo  Amezaliwa  Hapo  Ikiwemo  Kuingiza  Umeme  Uliopo  Kijiji Cha  Ikelu  Kwa  Gharama  Zake  Lengo  Kufikisha  Shule  Ya  Sekondari  Mtimbwi.

No comments:

Post a Comment