Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, September 4, 2015

NEW FORCE YAPINDUKA NJOMBE NA KUJERUHI 15

Majeruhi 15 Wamelazwa Katika Hospitali Ya Kibena  Kutokana Na  Ajali Iliyotokea Jana 

Majira Ya Saa Moja Usiku  Eneo La Mto Yakobi Ikilikutanisha Basi La Kampuni Ya New

Force  Lenye Namba Za Usajili   T 418 DDT Inayofanya Safari Zake Za Dar Es Salaama 

Songea  Kufuati Dereva Wa Basi Hilo Kuwa Na Mwendo Kasi.

Kamanda Wa Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Wilbroad Mutafungwa   Amethibitisha

Kutokea Kwa Tukio Hilo Na Kusema Kuwa Chanzo Cha Ajali Hiyo Ni Mwendo Kasi Wa

Dereva Wa Basi La New Force Na Loli Ambalo Lilikuwa Mbele Yake Lililokuwa

Limekwama Breki Na Kushindwa Kuweka Alama Barabarani.

Aidha Kamanda Mtafungwa Amesema Kuwa Basi Hilo La New Force  Lililokuwa

Likiendeshwa Na  Godfrey Mahenge Ambaye Naye Ni Miongoni Mwa Majeruhi 15 Liliacha

Njia Na Kutumbukia Mtoni  Na Kusababisha Majeruhi Hao  Baada Ya Kushindwa Kufunga

Breki Ghafra  Alipoona Mbele Yake Kuna Loli  Lenye Namba T 573 CDD.

Kamanda Mutafungwa Amesema  Dereva Wa Basi La New Force Anahojiwa Licha  Yakuwa

Anaendelea Kupata Matibabu Huku  Dereva Wa Loli  Namba T 573 CDD  Aina Ya Enveko

Mali Ya Kampuni Ya Otawa Akitafutwa Baada Ya Kukimbilia Kusikojulikana Ambapo Jeshi

La polisi Likiwataka Wamiliki Na Madereva Kuzingatia Sheria Za Usalama Barabarani.

CUE....KAMANDA AJALI

Kwa Upande Wake Majeruhi Wakizungumza Wakiwa Katika Hospitali Ya Kibena Mapema

Leo Wamesema Kuwa Basi Hilo La New Force Lilikuwa Mwendo Kasi Na Kufanya Dereva

Kushindwa Kuhimili  Kusimama  Ghafra Mara Lilipoonekana Loli  Limesimama Mbele

Yake Likiwa Limekatika Breki Na  Kusababisha Kupinduka Kwa Basi Hilo.
CUE.....MAJERUHI

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Njombe Kupitia Kitengo Cha Usalama Barabarani Limekuwa

Likitoa Elimu  Ya Usalama Barabarani Kwa  Madereva Na Wamiliki Wa Vyombo Vya  Moto

Kupitia Kituo Cha Radio Uplands Fm Kila Siku Ya Juma Tano Asubuhi Lakini Bado

Inaonekana Sheria Hizo Kupuuzwa Na Madereva.

Tukio Hilo La Ajali Limetokea Ikiwa Ni Siku Chache Tu Zimepita Tangu Jeshi La Polisi

Kupitia Kitengo Cha Usalama Barabarani Kuadhimishi Kilele  Chake Ambacho Mgeni

Rasmi Alikuwa Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dtk Rehema Nchimbi Ambaye Alitaka Sheria

Za Barabarani Kufuatwa Na Madereva  .

No comments:

Post a Comment