Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, July 30, 2015

WAKULIMA WA MIKOA YA IRINGA,NJOMBE NA RUVUMA WANOLEWA NA SHIRIKA LA AGRA




FRANK MUHANDO NI MENEJA WA MRADI IBB NYANDA ZA JUU KUSINI


MKURUGENZI MTENDAJI WA ACTN AFRIKA MHANDIS SAID MKOMWA






 HAWA NI WASHIRIKI WASHIRIKI WA MAFUNZO YA KILIMO HIFADHI YALIYOTOLEWA NA SHIRIKA LA AGRA.
 MKUFUNZI WA MAFUNZO KWA WAKULIMA KANDA YA KUSINI DEOGRATIAS NGOTIO AKIWAELIMISHA WAKULIMA HAO




 WASHIRIKI WA MAFUNZO YA SIKU NNE WAKICHANGIA  HOJA NA KUULIZA MASWALI
 WALIOSHIRIKI MAFUNZO YALIOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA FM HOTEL NJOMBE






 WASHIRIKI WAKIWA KATIKA KAZI ZA MAKUNDI




Abiud Gamba Ni Mratibu Wa Mradi Wa Afrikani Conservation  Tillage Network {ACTN}


MGENI RASMI NA MKURUGENZI MTENDAJI WA ACT AFRIKAN CONSERVATION TILLAGE NETWORK SAID MKOMWA AKITOA HOTUBA YAKE WAKATI WA KUFUNGA MAFUNZO YA SIKU NNE KWA WAKULIMA HAO.







MGENI RASMI NA MKURUGENZI MTENDAJI WA ACT AFRIKAN CONSERVATION TILLAGE NETWORK SAID MKOMWA AKITOA HOTUBA YAKE WAKATI WA KUFUNGA MAFUNZO YA SIKU NNE KWA WAKULIMA HAO.

Wakulima Wa Kutoka Mikoa Ya Iringa,Njombe Na Ruvuma Leo Wamehitimisha Semina Ya Siku Nne Kwa Kupewa Masharti Ya Kwenda Kuwaelimisha Wakulima Wengine Ambao Hawajahudhuria Semina Hiyo Ili Kudumisha Kilimo Hifadhi Kwa Manufaa Yao Na Taifa Kwa Ujumla.

Mkurugenzi Mtendaji Wa Shirika La ACT Said Komwa Amesema Wa wakilishi Wa Wakulima Kutoka Mikoa Ya Nyanda Za Juu Kusini  Wanatakiwa Kutumia Kilimo HifadhiKi Kitakacho wapatia Mazao Yakutosha Pasipo Kuharibu Udongo Na Kupanda Mazao Mzunguko.

Aidha Bwana Komwa Amesema  Matumizi Ya Trekta Na Jembe La Kukokotwa Na Wanyama Inasababisha Kuharibu Ardhi Ambayo Hata Mkulima Akiweka Pembejeo Za Mborea Haitafanya Kazi Ipasavyo Na Hivyo Wanatakiwa Kutumia Kilimo Hifadhi Kwa Kutumia Masalia Ya Mimea.

Kwa Upande Wao Wakufunzi Wa Mafunzo Hayo Deogratias Ngotio Na Abiud Gamba Wameshauri Wakulima Waliopatiwa Mafunzo Hayo Kwenda Kuwaelimisha Ambao Hawajahudhuria Mafunzo Hayo Na Kuwa Makini Matumizi Ya Viwatilifu AMbavyo Vina Madhara Kwa Watumiaji.

Aidha Wakufunzi Hao Wamesema Kuwa Serikali Inapaswa Kusambaza Wataalamu Wa Kilimo Katika Maeneo Ambako Wakulima Wanapatikana Ili Kutengeneza Mashamba Darasa Na Kuwa Mfano Kwa Wakulima Wengine  Na Kuiga Kilimo Hifadhi Kwa Manufaa Yao.

Wakizungumza Washiriki Wa Semina Hiyo Wamepongeza Kwa Elimu Iliyotolewa Kwa Siku Nne Mjini Njombe Ambapo Wameelezea Changamoto Zinazowakabili Katika Kilimo Ikiwa Ni Pamoja Na Kukosa Soko La Mazao Wanayozarisha Kwa Maeneo Ya Ludewa Na Songea.

Miongoni Mwa Changamoto  Zinazowakabili Wakulima Hao Ni Pamoja Na Kukosekana Kwa Soko La Mahindi,Kulima Kilimo Cha Mazoea Na Ufugaji ,Huku Wakulima Wa Wilaya Ya Ludewa Wakisema  Katika Wilaya Hiyo Vitendo Vya Rushwa Hufanyika Ili Waweze Kuuza Mazao  Yao.

Semina  Hiyo Ya Siku Nne Iliyotolewa Na Shirika La Afrikani Conservation Tillage Network  Imeelezwa Kuwa Na Mafanikio Makubwa Kwa Wakulima Hao Endapo Watakwenda Kutekeleza Walioagizwa  Ya Kwenda Kufundisha Wakulima Wengine Kutumia Kilimo Hifadhi.


No comments:

Post a Comment