Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, May 29, 2015

WAZEE NJOMBE WA NUFAIKA NA MIKOPO YA SHIRIKA LA PADI, LEO WAFUATILIA MATIBABU BULE KWA WAZEE KWA MKURUGENZI NA KWA MKUU WA MKOA



WAZEE WA YAKOBI  WILAYANI NJOMBE WANUFAIKA NA MIKOPO YA MBUZI NA KUKU KUTOKA SHIRIKA LA PADI


HAWA NI WAZEE WA  KATA YA MTWANGO WAKIFURAHIA MIKOPO YA MBUZI ILIYOTOLEWA NA SHIRIKA LA PADI
MBUZI WANAOTOLEWA KWA WAZEE NA SHIRIKA LA PADI
HAWA NI WAWAKILISHI WA WAZEE  WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE NA WANGING'OMBE


MWENYEKITI WA  WAZEE POSTA KATI  PIA NI MWAAKILISHI WA WAZEE WA WILAYA YA NJOMBE NA WANGING'OMBE BWANA ANDREW  MHAGAMA

WAZEE AMBAO NI WAWAKILISHI WA WAZEE WA HALMASHAURI ZA WILAYA YA NJOMBE NA WANGING'OMBE

 MRATIBU SHIRIKA LA PAD MKOA WA NJOMBE BI.RACHEL STEPHAN AKIWA OFISINI KWAKE AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI LEO


OFISI YA SHIRIKA LISILO KUWA LA SERIKALI MKOA WA NJOMBE LA PADI ILIYOPO  MTAA WA CHAUGINGI


 NA MICHAEL NGILANGWA -NJOMBE

 Wawakilishi Wa Baraza La Wazee Katika Halmashauri Nne Za Wilaya Ya  Njombe Na Wanging'ombe  Wamelazimika Kutembelea Ofisi  Za Wakurugernzi Wa Halmashauri Hizo Ili Kutambua  Namna Huduma Za Matibabu Zinavyotolewa Kwa Wazee Katika Hospitali,   Vituo Vya Afya Na  Zahanati .

Akizungumza Na Uplands Fm Mwenyekiti Wa  Wazee Katika Mtaa Wa Posta   Kati Na Muwakilishi Wa Wazee Kwa Halmashauri Nne Za Wilaya Ya Njombe Na Wanging'ombe Bwana Andrew Mhagama  Amesema Kuwa Lengo Kubwa La Kutembelea  Ofisi Za Viongozi Hao Ni Kutaka Kufahamu Utaratibu  Na Hatua Zinazochukuliwa Kwa Baadhi Ya Watumishi Wa Afya Wanaotumia Kauli Mbaya Kwa Wazee Wanapokwenda Kupatiwa Matibabu.

Aidha Bwana Mhagama Amesema Kuwa   Kumekuwa Na Baadhi Ya Wazee Ambao Wanapoteza Maisha Kutokana Na Kukosa Matibabu  Ambapo  Amepongeza Kwa Ushirikiano Mkubwa Uliooneshwa Na Wakuu Wa Idara   Na Wakurugenzi Wa Halmashauri Zote Mbili Pamoja Na Katibu Tawala Mkoa Wa Njombe  Huku Akisema Kuwa Utekelezaji Wa Sera Ya Matibabu Bure Kwa Wazee Bado Haujapewa Kipaumbele.

Kwa Upande Wao Wajumbe  Na Wawakilishi Wa Wazee Wilaya Ya Njombe Na Wanging'ombe  Pamoja Na Kupongeza Serikali Kwa Kuunga Mkono  Sera Ya Kuwapatia  Wazee Matibabu Bure Katika Hospitali Pia Wamesema Kuwa Kunachangamoto Mbalimbali Ambazo Zimekuwa Zikiwakabili  Ikiwemo Kukosekana Kwa Dawa Kwenye Hospitali,Vituo Vya Afya Na Zahanati  Na Kusababisha Kwenda Kuzinunua Kwenye Maduka Binafsi.

Wamesema  Baraza La Wazee Linawaunganisha Wazee Wote Kujua   Na Kuweza Kudai Haki Zao  Ambapo  Wameomba Wazee Kujiunga Kwenye Baraza Hilo La Wazee Ili Kujua Haki Zao Katika Maeneo Mbalimbali  Huku Wakilishukuru Shirika Lisilo La Kiserikali La PADI Kwa Kuwasaidia Kuwapatia Misaada  Ikiwemo Kuhamasisha Wazee  Kuungana Na Kupatiwa Matibabu Bure Kama Sera Ya Serikali Inavyo Sema.

Kwa  Mujibu Wa Senza Ya Mwaka 2012  Halmashauri Ya Mji Wa jombe Inakadiliwa Kuwa  Na Wazee 7423,Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Ikiwa Na Wazee  4888,Makambako  Wazee 5348 Na Halmashauri Ya Wilaya Ya Wanging'ombe Ikiwa  Na Wazee 9224  Ambao Wote Wanastahili Kupatiwa Matibabu Bure.

No comments:

Post a Comment