Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, April 27, 2015

WANANCHI WA KIJIJI CHA ITAMBO TAARAFA YA LUPEMBE WILAYANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI

BAADHI YA VIONJGOZI WA KIJIJI CHA ITAMBO  PAMOJA NA WANANCHI WA KIJIJI HICHO WAKIWA KWENYE ZOEZI LA UWEKAJI JIWE LA MSINGI







MHANDIS WA MAJI WILAYA YA NJOMBE  WA UPANDE  WA KULIA  MWENYE SUTI NYEUSI SENGAYAVENE MKALIMOTO



WAZEE WA KIJIJI CHA ITAMBO WAKIWA  NA FURAHA KUBWA BAADA YA KUPATA MAJI

Mkuu Wa Wilaya Ya Njombe Bi.Sarah Dumba  Ameweka Jiwe La Msingi  Kwenye  Mradi Wa Maji  Unaotekelezwa Na Shirika La  Walemavu  Nyombo  Kwa Kushirikiana Na Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Pamoja Na Wananchi Wa Kijiji Cha Itambo Wenye Zaidi Ya Shilingi Milioni Mia Mbili Hadi Kukamilika Kwake.

Akizungumza Na Wananchi Wakati Wa Kuweka Jiwe La Msingi Kwa Niaba Ya Mkuu Wa Wilaya Ya Njombe Kaimu Katibu Tawala Wa Wilaya Bi.Anna Wikatye Amesema Kuwa  Mradi Huo Uliowekewa Jiwe La Msingi Ni Ukombozi Kwa Wakazi Wa Kijiji Cha Itambo  Kupata Maji  Kwa Umbali Usiyozidi Mita 400  Kwa Mujibu Wa Sera Ya  Maji Ya Taifa Ya   Mwaka 2002.

Aidha  Bi.Wiketye Amesema Kuwa  Kukamilika Kwa Mradi Huo Kutasaidia Kupunguza Muda Mwingi Uliokuwa Ukipotea Kwa Akina Mama  Kuyafuata Maji Kwenye Milima Na Mambonde  Ambayo Siyo Safi Na Salama Ambapo  Kwa Sasa Wananchi Watashiriki Kikamilifu Katika Uzarishaji  Mali Na Kukuza Uchumi Wa Kila Mmoja.


Kaimu Mkurugenzi  Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Ambaye Ni Mhandis Wa Maji Sengayavene Mkalimoto  Pamoja Na Kuwapongeza Wananchi Kwa Kuunga Mkono Jitihada Za Serikali Na Shirika La Walemavu Nyombo  Kupitia Wafadhili Kutoka Hispani Wa Manos Unidas  Katika Kuwafikishia Maji Lakini Pia Amesema  Wananchi Wamechangia Zaidi Ya Milion 34, Halmashauri Imechangia Zaidi Ya Milioni 50 Huku Shirika Hilo Likiwa Limepeleka Zaidi Ya Shilingi Milioni Mia 119 Kukamilisha Mradi Huo.


Emmanuel Haule Ni Katibu Wa Shirika La Walemavu Nyombo Akisoma Risala Fupi Ya Utekelezaji Wa Mradi Huo Amesema  Hadi Sasa Shirika Limekamilisha Shughuli Za Ujenzi Wa Inteki,Njia Kuu Yenye Urefu Wa  Kilomita 10.9,Chemba Za Valvu,Wash  Out Na  Tenki Moja La  Lita  elfu 45000 Ambapo Kwa Sasa Wanatengemea Kuendelea Na Ujenzi Wa Tenki   La Pili,Njia Za  Kusambaza Maji Kilomita 5.1 Pamoja Na Jumla Ya Vituo Vya Bomba 19.


Kwa Upande Wao Wananchi Wa Kijiji Cha Itambo Kata Ya Mfriga Wameshukuru Shirika La Walemavu Nyombo Kuwasaidia Kupeleka Maji Kwa Kushirikiana Na Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Ambapo Wamesema Kwa Muda Mrefu Hawajawahi Kupata Maji Hayo Tangu Kuanzishwa Kwa Kijiji Hicho Na Kupata Hati Ya Usajili Wake Mwaka 1974  Akina Mama Hutegemea Maji Ya Mabondeni.

Mradi Huo Umewekewa Jiwe La Msingi Ikiwa Ni Kutekeleza Sera Ya Maji Ya Taifa Ya Mwaka 2002  Ya Kuwafikishia Huduma Hiyo Kwa Wananchi Vijijini Ambapo Katika Wiki La Maji Ambalo  Kilele Chake Kilifanyika  Machi 22 Mwaka Huu  Yakiwa Na Kauli Mbiu Isemayo  Maji Kwa Maendeleo Endelevu Ambayo Inatokana Na  Kauli Mbiu Ya  Siku Ya Maji Duniani Ya Mwaka 2015  Na Kwamba Bila Maji  Hakuna Maendeleo.











No comments:

Post a Comment