Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, November 17, 2014

DIWANI KAGUO AWAKUNA WAPIGA KURA WAKE MAKUNGU



diwani wa kata ya makungu Mgololo Yohanis cosmas kaguo


KWA HISANI YA FRANCIS GODWIN IRINGA


Diwani wa kata ya Makungu Mgololo Yohanis cosmas kaguo amesema  tatizo la miundo mbinu  katika kata yake limepungua kwa asilimia kubwa
Akizungumza  na mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz amesema kuwa amejitahidi kutoa  elimu  kwa wananchi na kujenga majengo mbalimbali ya kisasa katika shule za sekondari na shule za msingi.
kaguo ametaja baadhi ya majengo waliojenga ni pamoja na madarasa ,vyoo,viwanja  vya michezo  na kuzipa shule zote za eneo hilo vifaa vya michezo,  ujenzi wanyumba za walimu pamoja na maabara katika shule mbili za sekondari zizopo katika kata hiyo
 Aidha kaguo amesema kuwa katika kata ya makungu wametimiza lengo la rais wa jamuhuri ya muungano wa  tanzania dr jakaya mrisho kikwete kwa kujenga maabara katika shule zote mbili za kata hiyo kwa kujenga maabara zenye vyumba vitatukwa kila sekondari  vilivyo na ubora wa kitaifa 
Hivyo kutimiza lengo la wanafunzi wa kata hilo kusoma huku wakiwa na maabara za kisasa na zenye kiwango cha kitaifa na kuwafanya wanafunzi kusoma masomo ya sayansi kwa kuwa maabara za kufanyia mazoezi katika masomo yao tayari zimepatika na kuwaomba wanafunzi hao kusoma kwa juhudi masomo ya sayansi .
Pia diwani kaguo amewashuku wananchi wa kata hiyo ya makungu iliyopo mgololo kwa kuitikia wito wa ujenzi wa maabara na kushiriki katika kazi mbalimbali za kimaendeleo ambapo wamempa moyo wa yeye kujituma zaidi na kuwatumikia wananchi katika kuleta maendeleo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment