Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, April 13, 2013

Lwakatare aligawa Bunge


LISSU APANGUA TUHUMA ZA MWIGULU KWA CHADEMA
SAKATA la Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare na Ludovick Rwezaula kushtakiwa kwa makosa ya ugaidi, limeibua mvutano mkali bungeni huku wabunge wakishambuliana kwa maneno makali.
Mvutano huo uliibuka jana wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2013/2014 ambapo Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (CCM) alichafua hewa wakati akichangia na kudai kuwa aliyerekodi video ya Lwakatare yupo tayari kuja kutoa ushahidi.
Mwigulu ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) aliliambia Bunge kuwa CHADEMA wasihangaike kujitetea kwa swala la Lwakatare kwani ushahidi wote kuhusu video hiyo upo na kwamba yuko tayari kuutoa bungeni, duniani na mbinguni.
“Nataka nitoe ufafanuzi kuhusu suala la ugaidi ambalo Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amezungumza kwenye hotuba yake hapa bungeni jana. Aliyerekodi mkanda yupo na mimi niko tayari kuhojiwa popote hata mbinguni,” alisema Mwigulu na kuibua nderemo kutoka kwa wabunge wa CCM.
Mwigulu alionyesha karatasi aliyodai kuwa ilitumiwa na Lwakatare kupanga kile alichodai kuwa ni mkakati wa mauaji akisema huo ndiyo mkakati wa CHADEMA kupanga mauaji na kwamba viongozi wakuu wa chama hicho wanapaswa kushtakiwa.
Bila kujali kwamba suala hilo liko mahakamani wala ni kinyume cha kanuni za Bunge kumtaja mbunge mwingine kwa jina akimtuhumu, Mwigulu alisema anaishangaa CHADEMA kumtaka yeye aunganishwe kwenye kesi kwa kuwa na mawasiliano na mmoja wa watuhumiwa wakati hata wao wana mawasiliano na Lwakatare.
“Alisema Mbowe hapa jana kuwa mimi napaswa kushtakiwa kwa ugaidi, ingawa simuoni hapa ndani labda tayari amekwishakamatwa na polisi, lakini nataka kusema kuwa watu hawa ni waongo na wanafiki. Wanapanga mauaji halafu wanakuja hapa kuwahadaa wananchi kuwa wanapinga ugaidi,” alidai.

No comments:

Post a Comment