Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, January 6, 2017

Gambo apania kutokomeza vifo vya mama na Mtoto Mkoani Arusha

Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akizungumza katika mkutano wa Wadau wa Afya uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya Meru,kushoto ni Mganga Mkuu wa mkoa,Dk frida Mokiti.

Nteghenjwa Hosseah, Arusha

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Dokta Frida Mokiti amesema kuwa uhaba wa vituo vya afya katika maeneo ya pembezoni mwa miji umekua ukichangia vifo vya mama wajawazito na watoto kutokana na kutembea umbali mrefu kutafuta huduma hiyo.

 Akizungumza katika Kikao kazi cha Mkoa kinachojadili hali ya afya ya mkoa, Dr. Mokiti amesema kuwa juhudi za makusudi zinahitajika kuhakikisha kuwa huduma za afya kwa mama na mtoto zinapatikana kwa urahisi ili kupunguza tatizo hilo ambalo limekua likirudisha nyuma afya ya wakina mama pamoja na kukatisha maisha yao.

 Akizungumza katika Kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha kuwa wanajenga Kituo cha Afya katika kila tarafa ili kusogeza karibu huduma za afya kwa wananchi pia amewataka viongozi kuweka mipaka katika maeneo ya zahanati ili kuepuka uvamizi wa maeneo hayo yanayowahudumia watu.

“Wakati sasa umefika wa kuhakikisha tunatokomeza kabisa changamoto hii ya vifo vya mama na mtoto, inasikitisha sana kuona mama anafariki wakati wa kujifungua kwa sababu tu amekosa huduma ya afya karibu na makazi yake,lazima tuwalinde na kuwajali wananwake, kwa sababu bila ya wao kujifungua hata sisi tusingekuwepo” Alisema Gambo.

Aliongeza kuwa Kila Halmashauri ihakikishe inatenga Fedha kwenye mapato yake ya ndani halkadhalika Ruzuku toka Serikali Kuu ielekezwe kwenye Miradi ya Afya na tuendelee kutafuta wadau watakaotusaidia katika utekelezaji wa miradi hii bila kusahau uhamasishaji wa nguvu za wananchi kwa Pamoja tutatokomeza tatizo hili.

 Kwa upande wake Mkazi wa Arusha   Hussein Igunge na Mkuu wa Wilaya ya  Longido Mhe. Daniel Chongolo  wameitaka serikali iboreshe huduma za afya ikiwemo upatikanaji wa madawa kwa wale waliokata bima ili waweze kunufaika na bima zao pamoja na uhaba wa watumishi katika sekta ya afya.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Arusha,Dk Frida Mokiti akizungumza katika mkutano wa Wadau wa Afya uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya Meru,kulia ni Mkuu wa mkoa,Mrisho Gambo akimsikiliza kwa makini,kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Karatu na Katibu Tawala mkoa wa Arusha,Richard Kwitega.
Baadhi ya Watalaam wa sekta ya afya wakiwa kwenye mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya Meru mkoa wa Arusha.
Baadhi ya viongozi wa dini walioshiriki mkutano huo wakisikiliza kwa makini pia waliahidi kushirikiana na mfuko wa Bima ya Afya(NHIF)kuhamasisha waumini wao kujiunga na mfuko wa CHF.
Wakuu wa wilaya za mkoa wa Arusha wakiwa kwenye mkutano huo uliojadili kwa kina mikakati ya kuinua sekta ya Afya kutoka kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro,Mkuu wa wilaya ya Monduli,Idd Kimanta na Mkuu wa wilaya ya Karatu,Theresia Mahongo.

No comments:

Post a Comment