Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, January 6, 2017

BABU TALE ; Q CHIEF KAJA KUTEMBEA TU WASAFI


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Meneja wa mwanamuziki wa anayefanya vizuri katika soko la muziki wa bongo fleva nje na ndani ya nchi, Naseeb Abdul ‘Diamond’ , Hamisi Taletale ‘Babu tale’ amekanusha taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vya habari kuwa msanii Q Chief Kajiunga na kundi la wasafi.

Babu tale amesema hayo alipokuwa akizungumza na ripota wa globu ya jamii juu ya taharifa za msanii huyo kujiunga na WCB.

“Ninachokwambia mimi kama Meneja kuwa Q Chief kaja kutembea tu kama wanavyokuja kutembea wasaniii wengine, hivyo kuonekana pale sio ndio tunataka kumsajili tuwe nae,wasafi kama wasafi itabaki na watu wale wale” amesema Babu tale.

WCB ni kundi la muziki liliasisiwa na Msanii wa Bongofleva almaarufu kwa jina la Diamond, liomeonesha kuwa na mafanikio makubwa katika kipindi kifupi kwa kuwezesha wasanii wa hapa nchini kufanya kazi kimataifa kuliko ilivyozoeleka awali.

Katika kipindi cha mwaka 2016 kundi hilo limefanikiwa kuwasajili wasanii wengine kadhaa akiwemo msanii Rich Mavoko pamoja na Harmonize ambaye kwa sasa wote wanafanya vizuri.

No comments:

Post a Comment