Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, October 10, 2016

MKUU WA WILAYA LUDEWA ASIMAMISHA BODI YA SACCOS MLANGALI


 

 MKUU WA WILAYA YA LUDEWA  ANDREA  T'SELE
 

MKUU WA WILAYA  YA LUDEWA  ANDREA TSERE  AKISALIMIANA NA MADIWANI WALIOKUWEPO KWENYE KIKAO HICHO
MWENYEKITI WA SACCOS MLANGALI WA MUDA NATHANAEL  MGANI AKITOLEA UFAFANUZI KWA BAADHI YA  VIPENGELE  VYA KWENYE KATIBA YA CHAMA HICHO


DIWANI KATA YA MLANGALI AKIZUNGUMZA MBELE YA MKUU WA WILAYA KWENYE KIKAO CHA WANACHAMA WA SACCOS YA MLANGALI

MKUU HUYO WA LUDEWA TSERE AKIAGIZA KUCHUKULIWA HATUA KALI ZA KISHERIA WALIOHUSIKA NA ULAJI FEDHA ZA CHAMA CHA AKIBA NA MIKOPO










HUYU NI MWENYEKITI WA BODI YA SACCOS YA MLANGALI  WILLY HAULE AKIWA KWENYE KIKAO HICHO


KULIA NI MENEJA WA SACCOS YA MLANGALI  OSWARD MSAFIRI NA KUSHOTO NI MWENYEKITI WA SACCOS WILLY HAULE WAKITUHUMIWA KUHUSIKA NA UPOTEVU WA FEDHA ZA SACCOS HIYO PAMOJA NA WENZAO AMBAO HAWAPO HAPA





LUDEWA

Mwenyekiti wa bodi ya saccos mlangali na meneja wake wanashikiliwa na jeshi la  polisi Wilaya ya Ludewa  kwa tuhuma za kutumia vibaya  fedha na mali za chama cha ushirika cha akiba na mikopo cha mlangali .

Mkuu wa wilaya ya Ludewa Andrea Tsere ameagiza watuhumiwa Willy Haule ambaye ni mwenyekiti wa bodi na Osward Msafiri meneja wa saccos ya mlangali kushikiliwa kuanzia jana hadi hapo uchunguzi utakapo kamilika wakiwa gerezani kwa tuhuma za upotevu wa mali za chama ikiwemo misitu ya miti.

Kufuatia kushikiliwa na jeshi la polisi kwa watuhumiwa hao Bwana Tsere amelikabidhi jeshi la polisi saccos ya mlangali kuilinda na kuchunguza mali zote za chama wakishilikiana na viongozi wa muda wa bodi ya saccos hiyo wakati watuhumiwa wakiwa rumande hadi tarehe ndani ya mwezi mmoja  na wakibaini ubadhilifu  umefanywa na viongozi hao watafikishwa mahakamani
kujibu tuhuma zinazowakabili.

Aidha Tsere ametumia fursa hiyo kuliagiza jeshi la polisi kuwasaka wanachama wasiyofika kwenye mkutano wa chama na ambao wanadaiwa na saccos ikiwa hawajarejesha deni wanalodaiwa ili warejeshe fedha hizo ndani ya siku 30 huku akiagiza kumtafuta popote alipo mhasibu wa chama hicho aunganishwe na viongozi wenzake.

Wakijitetea mbele ya mkutano mkuu watuhumiwa wa sakata hilo Willy Haule mwenyekiti wa bodi na Osward Msafiri Meneja wa saccos ya Mlangali wamekana kuhusika na tuhuma za ubadhilifu wa fedha hizo kwa madai zilipotea wakati akiwa meneja marehemu Ludrof Chaula maarufu kacheche ambaye alikuwa diwani aliyefariki kwa kujinyonga mwaka 2012 baada ya kugudua dosari ya shilingi milioni 42 za chama hicho.

Wanachama wakiwa kwenye mkutano mkuu waemesema pesa nyingine zilizopotea ni za ufuatiliaji wa madeni ya wanachama waliokopa ambao walikuwa bado hawajarejesha deni lao huku riba ikiwa mara mbili ya mkopo wake.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya Andrea Tsere
ameivunja bodi na watumishi wa chama cha ushirika cha akiba na mikopo cha mlangali kutokana na viongozi wake kutuhumiwa kutumia vibaya fedha za chama hicho.

Bwana Tsere ametoa Uamuzi huo wa kuivunja bodi na kufukuza watumishi wa saccos hiyo baada ya kusikiliza malalamiko ya wanachama zaidi ya tisini wakiwatuhumu viongozi  wao kuhusika na ubadhilifu wa fedha zaidi ya shilingi milioni mia moja.

Aidha Tsere amewatoa hofu  wanachama wa saccos ya mlangali kwamba hakuna mwanachama yeyote atakayedhulumika haki zake zilizopo kwenye chama hicho  na kuitaka bodi ya muda iliyoundwa kusimamia saccos hiyo isifutwe kuhakikisha baada ya tarehe 30 mwezi novemba inaanza kazi ya kuendesha shughuli zake kama kawaida.

Awali Mwenyekiti wa muda wa bodi ya saccos ya mlangali  Nathanael Mgani  amesema wanachama wa saccos hiyo wamewiwa kumshilikisha mkuu wa wilaya hiyo katika kutafuta ufumbuzi wa migogoro inayowakabili baada ya kuona fedha walizoweka kwenye chama chao zimeliwa na watu wachache.

Baadhi ya wanachama wa saccos mlangali  wamelalamikia viongozi  wao kwa kudhuruma fedha za chama pamoja na kuwakata fedha za amana,fedha za hisa za wanachama kinyume na utaratibu.




No comments:

Post a Comment