Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, September 25, 2016

WAZEE KATA YA MAKOGA WALIA NA PENSHEN NA VITAMBURISHO VYA MATIBABU BURE






 WA UPANDE WA KULIA  NI MWENYEKITI WA SERIKALI YA KIJIJI CHA NG'ANDA NA WA KATIKATI NI DIWANI ALIYEKUWEPO KWA NIABA YA MBUNGE WA JIMBO LA WANGING'OMBE  Danroad  Mgaya  NA WA TATU NI MWENYEKITI WA BARAZA LA WAZEE KATA YA MAKOGA  Lutengano Mgaya


 Lutengano Mgaya MWENYEKITI WA BARAZA LA WAZEE MAKOGA AKIMKARIBISHA MGENI RASMI KWENYE SHEREHE ZA WAZEE



 WAZEE MBALIMBALI WA KUTOKA VIJIJI SABA VYA KATA YA MAKOGA WAKIWA KWENYE SHEREHE ZA WAZEE ILIYOFANYIKIA KIJIJI CHA NG'ANDA





 BURUDANI YA NGOMA NAYO IKACHUKUA NAFASI YAKE



Serikali  imetakiwa    kuchukua hatua kali dhidi ya wanaohusika  na  matukio ya mauaji kwa wazee  ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo  ambao wanapatikana katika vijiji mbalimbali  Mkoani Njombe.

Rai hiyo imetolewa na wazee wa  kata ya makoga wakiwa   kwenye sherehe yao iliyofanyikia katika kijiji cha Ng’anda  Wilayani Wanging’ombe ambapo wametoa kilio hicho kwa serikali  ili iwatatuliye  ikiwemo kupewa huduma za matibabu bure.

Aidha wazee hao kupitia risala iliyosomwa na afisa mtendaji Alberto  mpwaga wameshukuru shirika la PADI  Ambalo limekuwa likiwapatia mikopo midogo kwaajili ya kuendesha shughuli za miradi ya ufugaji  kuku,nguruwe na  kilimo  cha bustani huku akibainisha baadhi ya changamoto zinazowakabili kuwa ni kukosa  mfuko wa kujiendeleza.

Akizungumza na baadhi ya wazee wa kata ya makoga kwa niaba ya mbunge wa jimbo hilo diwani wa kata ya makoga  Danroad  Mgaya  ameomba kila kijiji kifanye kazi ya kufungua akaunti za benki na kuahidi kuzifikisha sehemu husika changamoto zilizowasilishwa na wazee kwenye sherehe hizo.

Awali Mwenyekiti wa baraza la wazee kata ya Makoga Lutengano Mgaya  ameshukuru uongozi wa kata ya makoga kwa kuonesha ushirikiano kwa kundi la wazee waliopo kwenye kata hiyo  na kusema baraza la wazee kata ya makoga linahamasisha vijana kuzingatia maadili ili kutunza utamaduni wa kila jamii.

Kwa upande wao baadhi ya wazee wameomba kuboreshewa huduma za matibabu katika maeneo yao kwa kuwatengenezea vitamburisho vitakavyowaruhusu kupatiwa  huduma za matibabu popote watakapo kwenda huku wakishukuru kwa jitihada zilizofanywa hadi sasa kwani baadhi yao wanapata huduma za matibabu bure.

No comments:

Post a Comment