Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 25, 2016

WATALAAMU WA HALMASHAURI WILAYA YA NJOMBE WATAKIWA KUTEMBELEA MAENEO YAO YA KAZI SIYO KUKAA MAOFISINI




Watalamu Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Wametakiwa Kuyatembelea Maeneo Mbalimbali Ya Utekelezaji Wa Majukumu Yao  Na Siyo Kukaa Ofisini Wakisubiri  Waitwe  Na Madiwani Wa Kata Zilizopo Wilayani Humo  Ndipo Wafike Sehemu Zao.

Mkuu Wa Wilaya Ya Njombe Ruth Msafiri  Ameitoa Rai Hiyo  Hivi Karibuni    Wakati  Akiongea   Na   Madiwani Wa Halmashauri Hiyo Kuhusiana Na Utekelezaji Wa Majukumu Ya Wataalamu  Kwa Wananchi  Walioko Vijijini .

B. Msafiri Amesema Ni Wajibu Wao Watalaamu Kuwatembelea Wananchi Lakini Siyo Kukaa Maofisini Wakisubili Waitwe Na Madiwani  Kwenda Kutatua Changamoto Zinazowakabili Wananchi  Na Kusema Hilo Ni Agizo Kwa Kila Mtumishi  Kuyafikia Maeneo  Ya Kazi Siyo Kuitwa Na Kila Kata Iwe Na Mtalamu Mmoja.

Mwenyekiti Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Valentino Hongori Amekili Kuwepo Kwa Tatizo La Baadhi Ya Watumishi  Ambao Wanasubili  Wapate Malalamiko Kutoka Kwa Viongozi  Wa Vijiji  Ambapo Amelazimika Kumuagiza Mkurugenzi Kusukuma Wataalamu Wayafikiye Maeneo Ya Vijijini.

Bwana Hongori Amesema  Uwajibikaji Wa Watumishi  Itaisaidia  Halmashauri  Hiyo  Kufanikiwa Katika Uzarishaji  Na Ukusanyaji Wa Mapato  Kutoka Kwenye Vyanzo Vyake  Kwa Kutoa Elimu Za Uibuaji Miradi Mipya Ya Wananchi.

No comments:

Post a Comment