Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 25, 2016

JESHI LA POLISI LUDEWA LAWATAKA WANANCHI KUONESHA USHIRIKIANO KUFICHUA WAHARIFU

Jeshi La Polisi Wilaya Ya  Ludewa   Mkoa Wa Njombe Limewataka Wananchi Wilayani Humo  Kuonesha Ushirikiano Kwa Jeshi Hilo Kwa  Kutoa Taarifa Za Uharifu  Ambao Unafanywa Na Askali  Polisi  Dhidi Ya Wananchi Kinyume Na Sheria.

Rai Hiyo Imetolewa Na Kamanda Wa Polisi Wilaya Ya Ludewa  Emmanuely Gariyamoshi  Wakati Akizungumza Na Wananchi  Wilayani Humo  Na Kusema Kuwa Amepokea Malalamiko Mengi Yanayohusu Askali Wake   Ambao Wamedaiwa Kufanya Kazi Kinyume Na Sheria Za Kiutumishi.

Kamanda  Gariyamoshi  Amesema Ili Kuhakikisha  Tabia Za Uovu Zinatoweka Miongoni Mwa Watumishi Wa Jeshi Hilo Ni Vema Wananchi Wakashiriki Kutoa Taarifa Kwa Kupiga Simu Au Kufika Katika Ofisi Za  Jeshi Hilo Wilaya  Ili Hatua Zichukuliwe Haraka  Kwa Wanaokwenda Kinyume.

Kauli Ya Kamanda Huyo Imekuja Ikiwa Ni Siku Chache Tangu Mkuu Wa Wilaya Ya Ludewa  Andrew Tsere Kulaani  Kitendo  Cha Askali Wa Kituo Cha Polisi Mlangali Kuwalaza   Watu Wanaofikishwa Kituoni Hapo Na Kuwatoza Fedha  Zilizo Kinyume Na  Maadili Ya Kazi Yao Ambapo Kamanda Huyo Ameahidi Kuwachukulia Hatua  za kisheria Askali  Waliohusika Na Tukio Hilo.

Kamanda GariYaMoshi  Amesema Jeshi Hilo  Litaendelea Kutoa Elimu Kwa Askali  Wake Juu Ya Utendaji Kazi Ili Kusitokee Tena Na Malalamiko Ya Wananchi Kuhusiana Na Askali Huku Akitoa Wito  Kwa Wananchi  Kuendelea Kuonesha Ushirikiano Kwa Jeshi Hilo Katika Kuwafichua Waharifu.

No comments:

Post a Comment