Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 25, 2016

MIUNDOMBINU YA BARABARA YA KIJIJI CHA IKANDO YAWA TATIZO KWA WANANCHI

Wananchi Wa Kijiji Cha Ikando Wilayani Njombe Wameitaka Serikali Kuboresha  Miundombinu Ya Barabara  Na  Afya  Ili Kuwanusuru  Wamama Wajawazito Wasitozwe Faini Ya Elfu 50 Wakijifungulia Njiani Wakati Wakienda Katika  Zahanati Ya Kijiji  Cha Ibumila.

Rai Hiyo Imetolewa Na Wananchi Wa Kijiji Cha Ikando Wilayani Njombe Wakati Wakizungumza Na Uplands Fm Kuhusiana Na Changamoto  Zinazowakabili  Ikiwemo  Tatizo La Kusafiri Umbali Mrefu Wa Kilomita Tano Kufuata Huduma Za Matibabu Zahanati Ya Ibumila.

Wamesema   Kero Hiyo  Imemufikia  Mbunge Wa  Lupembe Joramu Hongori   Kupitia Mkutano Wake Uliofanyika  Augost  8 Mwaka Huu  Na Kumpatia Kero  Mbalimbali Ikiwemo  Manesi Wa Zahanati Ya Ibumila Kuwatoza Faini  Elfu 50 Wajawazito Wakijifungulia Njiani Pasipo Kuzingatia Umbali Wanaosafiri .

Wananchi Hao Wamesema Changamoto Nyingine  Ni Kukosekana Kwa Madaraja,Maji  Na Barabara Rafiki Za  Kuunganisha  Vijiji Vya Ikando,Ibumila Na Vijiji Vya Kata Ya Igima Vya Igairo Na Lulanzi  Ili Kupata Urahisi Wa Kusafirisha Wagonjwa  Kuelekea Hospitali Ya Kibena Pamoja Na  Mazao  Hususani Msimu Wa Masika.

Mwenyekiti Wa Serikali Ya Kijiji Cha Ikando Kata Ya Kichiwa   Isack Mwinami  Amekili Kuwepo Kwa Tatizo La  Kukosekana Kwa huduma Ya Afya Kwenye Kijiji Chake  Na Kusababisha Akina Mama Wajawazito Kujifungulia Njiani  Na Wakifika Kwenye Zahanati Ya Kijiji Cha Jirani Kuwa Toza Faini Ya Elfu 50  Tatizo Lililokuwepo Hapo Hawali Lakini Siyo Kwa Sasa.

Mwinami  Amesema kutokana Na Kuwepo Kwa Tatizo La Kukosekana Kwa Huduma Za Afya  Kwenye Kijiji Hicho  Jitihada Zimeanza Za Ujenzi Wa Zahanati Ya Kijiji  Ili Kurahisisha Huduma Za Afya Kwa Wananchi  Huku Akisema Zahanati Iliyopo  Inatatizo La Kukosa  Dawa  Na Kusababisha Wagonjwa  Kununua Kwenye Maduka Ya Watu Binafsi.

No comments:

Post a Comment