Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 25, 2016

UMOJA WA WAUZAJI NA WAMILIKI WA MADUKA YA DAWA MUHIMU WATEUWA VIONGOZI WA MUDA NJOMBE



Umoja Wa Wauzaji Wa Maduka Ya Dawa Mjini Njombe  UWAMADANJO  Leo Umefanikiwa Kuteuwa Viongozi  10 Wa  Muda  Ambao Watasikiliza Kero Za Wanaumoja Huo Na Kuziwasilisha Sehemu Husika Kwaajili Ya Kupatiwa Ufumbuzi.

Akizungumza Na Uplands Fm Mara Baada Ya Kufanyika Kwa Kikao Cha Kufanya Uteuzi Huo Mwenyekiti  Aliyeteuliwa  Paul Masasi  Amesema Lengo La  Umoja Huo Ni Pamoja Na Kuboresha Huduma  Za Utoaji Dawa Kwa Kila Muuzaji Na Kudhibiti  Uuzwaji Dawa Kiholela.

Bwana Masasi Amesema Umoja Huo Utahakikisha Unafuatilia  Baadhi Ya Wamiliki Wa Maduka Na Wauzaji Wake  Kuhakikisha Wanakuwa Na Vyeti Halali  Na Siyo Vya Kugushi Pamoja Na  Dawa Ambazo Zimesajiliwa Kisheria  Ambapo Kinyume Na Sheria  Uongozi Utachukua Hatua Za Kufikisha Kwa Mfamasia .

Kwa Upande Wake  Muwakilishi Wa Baraza La  Famas Ambaye  Pia Ni Mfamasia Wa Halmasahuri Ya Mji Wa Njombe Simon Kwama  Amesema  Wamiliki Wa Maduka Ya Dawa  Wanatakiwa Kuzingatia Kanuni Na Sheria Kwa Mujibu Wa Usajili Wa Duka Lake Ikiwemo Kutochanganya  Maabara Na Duka La Dawa Sehemu Moja.

Mfamasia Huyo Amesema Kuundwa  Kwa Umoja  Wa Wauzaji Wa Dawa Mjini Njombe  Kutasaidia Miongoni Mwao Kuondokana Na  Ukiukwaji Wa Kuuza Dawa Hizo Na Kutaka  Wamiliki Wa Maduka Hayo Kuzingatia Kanuni Na Sheria Walizopewa Kwa Mujibu Wa Leseni Zao.

Baadhi Ya Wamiliki Wa Maduka Walioshiriki Kwenye Kikao Hicho Kilichofanyikia Ukumbi Wa Miliam Hotel  Wamesema Umoja Huo Utawasaidia Kutatua Changamoto Mbalimbali  Ikiwemo Kudhibiti Wanauza Dawa Kwenye Maduka Ya Bidhaa Nyingine Za Vyakula Na Kuwasilisha Kero Zinazowakabili.

No comments:

Post a Comment