Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 25, 2016

AJALI ZAENDELEA KUJITOKEZA NJOMBE

Wamiliki Na Madereva Wa Vyomba Vya Moto Mjini Njombe Wametakiwa Kuondoa Uzemba Wakati Wakiwa  Barabarani  Na Kuacha Kuendesha Chombo Cha Moto  Wakiwa Hawana Uwezo Wa Kuendesha Kwenye Barabara Kuu  Na Kufanyia Matengenezo  Vyombo Vyao.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Diwani Wa Kata Ya Njombe Mjini   Agrey Mtambo Akiwa Miongoni Mwa Mashuhuda Wa Tukio La Ajali Iliyotokea Majira Ya Saa Kumi Na Mbili Na Dakika 45  jioni Ya Jana Augost 23  Katika Eneo La Njia Panda Ya Magereza Ambapo Gari Yenye Namba Za Usajiri T 407 CJM yenye rangi nyeupe ililigonga ubavuni Gari lenye namba T 995 CUX .

Bwana Mtambo Amesema Matukio Ya  Ajali Yamekuwa Yakitokea Kutokana Na Uzemba Wa Baadhi Ya Madereva Wakiwa Barabarani  Ambapo Ametolea Mfano Wa Ajali Iliyotokea Jana Jioni Katika Eneo La Njia Panda Ya Magereza  Ambayo Imesababishwa Na Dereva Aliyekuwa Akitokea Barabara Ya Magereza Kuelekea Mjimwema Na Kuligonga Gari Lililokuwa Likitokea Barabara Ya Songea  -Njombe.

Awali Wakizungumza  Na Uplands Fm Baadhi Ya Mashuhuda Wa Tukio La  Ajali Hiyo Wamesema  Uzemba Wa Madereva Ndiyo Chanzo Kikubwa Cha Ajali Za Barabarani Ambapo Katika Ajli Hiyo Haikusababisha Kifo Wala Majeruhi Wowote Huku Wakipongeza Jeshi La Polisi Kwa Kufika Kuimarisha Usalama Wa Raia Katika Eneo La Tukio Lilipotokea.

Jeshi La Polisi Mkoani Njombe Limekuwa Likitoa Elimu Ya Usalama Wa Barabarani Kupitia  Uplands Fm Kila Siku Ya Juma Tano Na Kwenye Mikutano Mbalimbali Ya Hadhara Lakini Bado Matukio Ya Ajali Yameendelea Kujitokeza  Katika Maeneo Mbalimbali Mkoani Njombe.

No comments:

Post a Comment