Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, August 6, 2016

MKUU WA MKOA WA NJOMBE DKT REHEMA NCHIMBI AMUAGIZA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE KUHAKIKISHA ANAONDOA UCHAFU KWENYE VIZIMBA

 MKUU WA MKOA WA NJOMBE DKT NCHIMBI  AKIZUNGUMZA NA KUONEKANA KUKELWA NA UCHAFU ULIOPO KWENYE VIZIMBA NJOMBE MJINI IKIWA NI ENEO LA MAKAO MAKUU YA MKOA WA NJOMBE.


 HII NDIYO HALI YENYEWE ANAYOIPIGIA KERERE MKUU WA MKOA  WA NJOMBE DKT NCHIMBI NA HAPA NI MTAA WA MELINZE





HUU NDIO MRUNDIKANO WA UCHAFU KWENYE VIZIMBA  MITAA KARIBU YOTE YA NJOMBE MJINI HALI IKO HIVI. N

Na Michel Ngilangwa -Njombe

Licha Ya Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Kuwa Miongoni Mwa  Halmashauri Zilizopata Tuzo Ya  Ushindi   Katika Mashindano  Ya Afya Na Usafi Wa Mazingira  Nchini ,Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe  Dkt Rehema Nchimbi Ametoa Onyo Kwa  Halmashauri Hiyo   Kwamba  Inakabiliwa Na Tatizo La Uchafu  Na  Harufu Mbaya  Inayotokana Na Mkusanyiko Wa Taka Zilizopo Kwenye Vizimba  Mjini Hapa.

Akizungumza Na Wakuu Wa Wilaya ,Wakurugenzi,Wenyeviti Wa Halmashauri Na Baadhi Ya Wananchi  Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi Amemtaka  Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Iluminata Mwenda Kuhakikisha Anasimamia Zoezi La  Uondoaji Wa Taka Kwenye Vizimba  Vilivyopo Katika Maeneo Mbalimbali  Ya Sokoni Na Kwenye Makazi  Ya Watu.

Hatua Ya Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Nchimbi  Kumuagiza Mkurugenzi Huyo Imefuatia  Halmashauri Hiyo Kupewa Tuzo Ya Kikombe Na Pikipiki Moja  Kwaajili Ya Ushindi Wa Mashindano Ya Afya Na Usafi Wa Mazingira Licha Ya Mji Wake Kuwa Na Harufu Mbaya  Inayotokana Na Uchafu Wa Vizimba  Ambavyo Haviondolewi Takataka Zake Kwa Muda Murefu.

Alphan Ngulo Ni Mwenyekiti Wa Serikali Ya Mtaa Wa Joshoni Mjini Njombe  AAkizungumza  Na Uplands Fm Hapo Jana  Amesema Tatizo La Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Kushindwa Kuondoa Takataka Kwenye Vizimba Limekuwa  Ni La Muda Mrefu  Licha Ya Viongozi Wa Mitaa Kuwapatia Taarifa Za Kuwepo Kwa Taka Hizo Ikiwemo Kizimba Cha Soko  La Joshoni Ambacho Kina Takribani Miezi Sita  Hakijafanyiwa Usafi.

Kwa Upande Wake Wananchi Mjini Njombe  Wamelalamikia Kuwepo Kwa Tatizo La Kushindwa Kuondolewa Kwa Taka Kwenye Vizimba Kwa Muda Mrefu Huku Wakitolea Mfano Kizimba Cha  Mtaa Wa Sido Nyuma Ya Uwanja Wa Sabasaba,Nationalhousing,Buguruni Na Maeneo Mengine Ambayo Yanakabiliwa Na Changamoto Ya Uchafu Licha Ya  Kutozwa Hela Ya Uchafu.

.........................................................................

No comments:

Post a Comment