Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, August 6, 2016

RC NJOMBE AAGIZA KUWASAKA, KUFUNGIA BAR ZINAZOUZA MABARMED


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjHxzoRC27K-thYxjFWdlIR7XITZVy_pcQpUS7FgRVN7c6zljHZuSjBaz5emHDUCXOHNDync5NwESdPuZ_5-lVji1fUphf-TDfaPfWOU0JJutn52DSo4obrpaNmbhqbmRuD8igRSLB1IZwb/s1600/DSC_0896.JPG

 MKUU WA MKOA WA NJOMBE DKT REHEMA NCHIMBI 

Wakurugenzi Wa Halmashauri Za Mkoa Wa Njombe  Wametakiwa Kufanya Oparesheni  Ya Kuwakamata Na Kuwachukulia Hatua Za Kisheria Baadhi Ya Wamiliki Na Waajili Wa Wafanyakazi Wa  Biashara Za Pombe    Ikiwa Ni Pamoja Na Kuzifunga Bar Zote Zenye Mabamed Ili Kupunguza Maambukizi Ya Virusi Vya Ukimwi Mkoani Hapa Kwa Kipindi Hiki Cha Utawala Wa Rais Wa Awamu Ya Tano .

Agizo Hilo Limetolewa Na Mkuu Wa Mkoa  Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi Wakati Akizungumza Na Wakurugenzi  Wa Kutoka Halmashauri Sita Za Mkoa Wa Njombe Na Kutaka Wakurugenzi  Hao Kushirikiana Na Taasisi Nyingine Zisizo Za Kiserikali   Kutokomeza Tabia Ya  Baadhi Ya  Waajili Wa Wafanyakazi Wa Bar  Ambao Wanachukuliwa Sehemu Mbalimbali Kwa Lengo La Kuwauza Kigono.

Aidha Dkt Nchimbi  Ametolea Mfano Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Kwamba Kuna Bar  Ambazo Wamiliki Wake Wameajili Wafanyakazi  Wa Kuuza Pombe Hizo Na  Miili Yao Pasipo Wao Kukusudia  Huku  Mameneja Wengine Wakiwaweka Kwenye Mazingira Hatarishi  Wafanyakazi Hao  Kwa Kuwataka Wafanye  Matendo Maovu  Ya Kwenye Madanguro Yanayoashilia Kueneza Maambukizi Ya Virusi Vya Ukimwi.

Dkt Nchimbi Ametaka Kufungiwa Kwa  Bar Hizo Na Kuwachukulia Hatua Kali Mameneja Wanaoendekeza Biashara Ya  Ngono Kwa Kuwauza Mabinti Wa Bar Baada Ya  Wakurugenzi Hao Kufanya Msako   Wa Mabamedi  Wanaojihusisha Na  Vivutio Vya Ngono Na Kusababisha Maambukizi Hayo Kuendelea  Kueneo Kwa Mkoa Wa Njombe  Ambapo Wanatakiwa Kuvunja Mitandao Ya Kueneza Maambukizi Hayo.

Katika Hatua Nyingine Dkt Nchimbi Ametaka Wananchi,Wadau  Wa Elimu, Jeshi La Polisi  Kwa Kushilikiana Na  Taasisi Ya Kuzuia Na Kupambana Na Rushwa  Nchini Takukuru Mkoa Wa Njombe  Kuwa Karibu Na Maeneo Ya Shule  Za Msingi   Ili Kuwabaini  Baadhi Ya Walimu Wenye Mahusiano  Ya Kingono Na  Wanafunzi  Na Kuwachukulia Hatua Kali Za Kisheria Akiwemo Mwalimu Anayetuhumiwa  Kuwa Na Mahusiano Ya Kingono Na Wanafunzi 12 Wilayani Ludewa.

Agizo Lingine La Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi Ni Pamoja Na Maafisa Elimu Kutumia Baiskeli Kuzifikia Shule Wanazozisimamia  Endapo  Halmashauri Zao Zitakosa  Mafuta Ya Kuweka Kwenye Magari  Na Kuwatimua Walimu Wenye  Tabia Ovu  Shuleni Za Kingono Na Wanafunzi.

No comments:

Post a Comment