Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, August 5, 2016

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI IDINDILIMUNYO WANATUMIA VYOO VILIVYOEZEKWA KWA NYASI BAADA YA KUTITIA VYA AWALI MWEZI MACHI MWAKA HUU




 
 HIVI NI VYOO VYA MUDA WANAVYOTUMIA WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI IDINDILIMUNYO BAADA YA KUTITIA VYOO VYA AWALI MWEZI MACH MWAKA HUU



 HIVI NI VYOO VILIVYOTITIA MWEZI MACHI MWAKA HUU KATIKA SHULE YA MSINGI IDINDILIMUNYO
 WAZAZI WA KIJIJI CHA IDINDILIMUNYO  WAKALAZIMIKA KUANZA ZOEZI LA KUCHIMBA SHIMO NA KUANZA UJENZI WA VYOO VYA KISASA  NA LILIPOKUJA ZOEZI LA UCHANGIAJI MADAWATI  WAKAGOMA KUCHANGIA HADI WAKAMILISHI MRADI HUU WA VYOO VILIVYO SALIA KUWEKA MILANGO NA KUPAKWA RANGI





HAPA NI JIKONI WANAKOPATIWA CHAKULA WANAFUNZI WA SHULE HIYO



 HIVI NDIVYO VYOO WANAVYOTUMIA KWA SASA  KATIKA SHULE YA MSINGI IDINDILIMUNYO

 VYOO WALIVYOJENGA AMBAVYO BADO HAVIJAANZA KUTUMIKA VINA MASINKI NA KILA KITU KASORO MILANGO WANASEMA WANAENDELEA NA JITIHADA ZA KUKAMILISHA





HIVI NI VYOO VYA ZAMANI VILIVYOHARIBIKA KATIKA SHULE HIYO

Wananchi Wa Kijiji Cha Idindilimunyo Wilaya Ya Wanging'ombe Mkoani Njombe Wametishia Kugoma Kuchangia Michango Ya Madawati  Ili Kutekeleza Agizo La Rais Magufuli  Kwa Madai  Kuwa Hawawezi Kuchangia Miradi Miwili Kwa Wakati Mmoja  Nakwamba Hadi Wakamilishe Ujenzi Wa Vyoo   Kwaajili Ya Wanafunzi Wa Shule Ya Msingi Idindilimunyo Kufuatia  Vyoo Vya Zamani Kutitia Mwezi Mach Mwaka Huu.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Wananchi Wa Kijiji Hicho Wakati Wa Mkutano Wa Hadhara Uliofanyika Jana  Na Kusema Kuwa  Hawawezi  Kuchangia Madawati  Kwa Kipindi Hiki Ikiwa  Wanaendelea Na Ujenzi Wa Vyoo Vya Kisasa  Kwaajili Ya Wanafunzi Hao  Nakwamba Dhamira Yao Ni Kutaka Kuweka Mazingira Mazuri Ya Wanafunzi  Katika Kuelekea Kipindi Cha Mvua.

Aidha Wananchi Hao Wamesema Kuwa  Siyo Kwamba Wanakataa Kuchangia Madawati Hayo  Bali Jitihada Zao Wanazielekeza  Kwenye    Kipaumbele  Chao Kikubwa  Cha Tatizo La Wanafunzi Kukosa Vyoo  Kwani Hadi Sasa Wanatumia Vya Muda Vilivyoezekwa Kwa Majadi   Ambapo Ili Kuepukana Na Tatizo La Mlipuko Wa Magonjwa Ya  Kipindupindu Imewalazimu Kukamilisha  Ujenzi Huo Mwaka Huu.

Akizungumza Mara Baada Ya Kumalizika Kwa Mkutano Wa Hadhara Mwenyekiti Wa Serikali Ya Kijiji Cha  Idindilimunyo  Goden Kasanga  Ameutupia Lawama Uongozi Wa Halmashauri Ya Wanging'ombe Kwa Kushindwa Kulichukulia Uzito Swala La Kukosekana Kwa Vyoo Katika Shule Hiyo  Huku Akisema Serikali Ya Kijiji Hicho Inaungana Na Wananchi Kutochangia Madawati Kwa Mwaka Huu.

Kasanga Amesema Kuwa Hadi Sasa Serikali Ya Kijiji Kwa Kushilikiana Na Wananchi Wake Wamekamilisha Ujenzi Wa  Matundu 16 Ya Vyoo Vya Kisasa  Ambavyo Vimebakia Kuweka Masink   Vilivyo Gharimu Zaidi Ya Shilingi Milioni 20  Ikiwa Halmashauri Kupitia Idara Ya Elimu Haijashiliki Kupeleka Msaada Wowote  Kunusuru Afya Za Wanafunzi Wa Shule Ya Msingi Idindilimunyo Ambao Vyoo Vyao Vilititita Mwezi Mach Mwaka Huu.

Uplands Fm Imeshuhudia Vyoo  Vya Muda Vinavyotumiwa Na Wanafunzi  Kwa Sasa Vikiwa Vimejengwa   Kwa Majani  Baada Ya Vyoo Vya Zamani Kutitia Jambo Lililowalazimu Wananchi Na Serikali Yao Kuanza Mara Moja Jitihada Za Ujenzi  Huo.

No comments:

Post a Comment