Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, August 18, 2016

IDARA ZA AFYA ZA TAKIWA KUWA NA TAARIFA SAHIHI ZA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI


 WA UPANDE WA KULIA NI KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE JACKSON SAITABAHU,WA PILI KUTOKA KULIA NI MKUU WA MKOA WA NJOMBE DKT REHEMA NCHIMBI NA WA TATU KUTOKA KULIA NI MKUU WA WILAYA YA NJOMBE LUTH MSAFIRI WAKIWA KWENYE KIKAO CHA AFYA YA MSINGI CHA MKOA WA NJOMBE

HAWA NI WATAALAMU WA AFYA WA KUTOKA HALMASHAURI ZA MKOA WA  NJOMBE






 MKURUGENZI WILAYA YA WANGING'OMBE  BI.KIWANUKA AKIWA NA MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE ANTONY MAHWATA
 MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE ALLY KASINGE ALIYEVAA MIWANI WA KWANZA NA WA PILI NI MKURUGENZI HALMASHAURI YA MAKAMBAKO PAUL MALALA WAKIWA NA KIKOSI CHA JESHI LA POLISI KWENYE KIKAO CHA AFYA YA MSINGI



Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi  Amezitaka Halmashauri Kupitia Idara Za Afya Kuhakikisha  Zinatafuta Taarifa Sahihi Za Maambukizi Ya Virusi Vya Ukimwi   Pamoja Na Kutatua  Changamoto Zilizopo Na Namna Ya Kuzitatua.

Akizungumza Wakati Wa Kufungua Kikao Cha Kamati Ya Afya Ya Msingi  Akiwa Ni Mwenyekiti Wa Kikao Hicho Dkt Nchimbi Amesema Haikubaliki  Mkoa Wa Njombe  Unaopewa Sifa Kwa Kushinda Mashindano Mbalimbali  Kitaifa Na Kikanda Ukaongoza Kwa Maambukizi Ya Ukimwi Na Kutaka Wadau Na Wataalamu Kutafuta Suruhisho Lake.

Dkt Nchimbi   Amesema Kila Halmashauri Kupitia Idara Za Afya Zinatakiwa Kuandaa  Mikakati Mbalimbali Ya  Kufikia Maambukizi Sifuri Ifikapo Mwaka 2020  Na Maambukizi Ya Asilimia 3  Ndani Ya Mwaka Huu  Kwa Kupata Takwimu Zilizo Sahihi  Kwa Kuweka Kitu Cha Pekee Katika Sekta Ya Afya Na Siyo Kutekeleza Majukumu Yao Kwa Mazoea.

Dkt Nchimbi Bado Amerudia Kauli Yake Ya Kuzifungia Bar Zote Zinazoendesha Biashara  Zao Kinyume Na  Maadili Kwa Kuwauza  Wafanya Kazi Wao   Yaani Mabarmed   Ambao Wamedaiwa Kuchangia Maambukizi Ya UKIMWI Mkoa Wa Njombe Kutokana Na Uhamisho Wao Wa Mara Kwa Mara  Na Kuwaagiza Wakuu Wa Wilaya Kusimamia Zoezi Hilo Wakishilikiana Na Jeshi La Polisi.

Akiwasilisha Taarifa Ya Maambukizi Ya UKIMWI Mkoa Wa Njombe  Afisa Ustawi Wa Jamii Mkoa Wa Njombe  Bi. Teresia Yomo Amesema Kuna Njia Mbalimbali Ambazo Zinaweza Kuchangia Maambukizi Hayo Ikiwemo  Kunyoa Kwenye Saluni,Kutumia Pamoja Vitu Vyenye Nja Kali  Huku Akisema Kuna Waraka Ambao Unamuongoza Muajili Kumsaidia Mfanyakazi Kwa Kumpatia Elimu Na Kuwangezea Posho.

No comments:

Post a Comment