Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Saturday, August 20, 2016

DC WANGING'OMBE AWACHARUKIA WATUMISHI WALIOMLIPA MKANDARASI FEDHA TASLIMU BADALA YA HUNDI


 

MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE ALLY KASINGE AKITOA MAAGIZO KWA MKURUGENZI WA WANGING'OMBE MBELE YA WANANCHI WA KIJIJI CHA MNG'ELENGE 


 HILI NIN JENGO LA ZAHANATI YA KIJIJI CHA MNG'ELENGE  AMBAYO INAENDELEA NA UJENZI








 MKUU WA WILAYA YA WANGING'OMBE AKIZUNGUMZA NA MKANDARASI NODRICK DANIEL MNG'ONG'O ALIYEJENGA ZAHANATI HIYO NA KUPOKEA FEDHA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI NNE BADALA YA ZAIDI YA SHILINGI MILIINI TATU NJE YA MKATABA

 AFISA USHIRIKA WILAYA YA WANGING'OMBE GOODSON MTAMA AKIFAFANUA JUU YA CHAMA CHA AMCOS










DKT  JAMES LIGWA AKIWA KWA NIABA YA MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA WANGING'OMBE



 HUYU NI MWENYEKITI WA KIJIJI CHA MNG'ELENGE ALIYEKAIMISHWA KWA MUDA BAADA YA WA ZAMANI KUTENGULIWA NAFASI YAKE YA UONGOZI NA WANANCHI

 DIWANI WA KATA YA WANGING'OMBE GEOFREY NYAGAWA AKISHUKURU KWA KUFIKA MKUU WA WILAYA KUTOA UFAFANUZI

Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Ally Kasinge ameagiza kuwachukulia hatua za kinidhamu  watumishi  waliokiuka sheria za kumlipa pesa tasilimu mkandarasi aliyejenga zahanati ya Mng’elenge bila kumuandikia hundi kinyume na sheria.

Bw. Kasinge ametoa maagizo hayo katika mkutano wa hadhara kwenye kijiji cha Mng’elenge Kata ya Wanging’ombe wilayani wanging’ombe wakati akitoa mrejesho kufuatia malalamiko ya wananchi juu ya ujenzi wa zahanati ya kijii hicho.

Amesema kuwa watumishi wa Halmashauri hiyo wamefanya  malipo ya fedha kiasi cha  shilingi milioni 15 pasipo kuandika hundi kama sheria inavyowataka.

Kasinge amebainisha mapungufu mengine kuwa ni   kufanyika kwa manunuzi ya moja kwa moja bila kufuata sheria za manunuzi na kutumia kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 10 ikiwa sheria inawataka kufanya ushindanishi   wa manunuzi tofauti na wao walivyofanya.

Diwani Wa Kata Ya Wanging'ombe  Wilayani Wanging'ombe Geofrey Nyagawa  Amepongeza Wananchi Kwa Jitihada Walizofanya Za Kuwapigia Kelele Viongozi Na Hatimaye Ukweli Umepatikana Na Kutaka  Kurudisha Moyo Wa Kushiriki Shughuli Za Maendeleo Kama Zamani.

Zahanati ya kijiji hicho inatarajia kugharimu zaidi ya milioni 90 hadi kukamilika kwake  ambapo  Halmashauri imechangia  kiasi cha milioni 15 huku nguvu za wananchi zikiwa ni zaidi ya milioni 8 na kufikia  zaidi ya shilingi  milioni 23 hadi ilipo fikia hatua ya upauwaji.

No comments:

Post a Comment