Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Monday, August 22, 2016

UMOJA WA MADEREVA WA MAGARI YA SERIKALI WILAYA YA NJOMBE WAMUAGA DEREVA MWENZAO KWA KUSTAAFU








 MADEREVA WENZAKE WAKIMPOKEA NJE YA UKUMBI WA HALMASHAURI YA WILAYA  MWENZAO ANAYESTAAFU PHED NDALE



 HAPA NI BAADHI YA MADEREVA WAKIWA NA AFISA MIPANGO BI. WAZA NA AFISA UTUMISHI AMBAYE NI MGENI RASMI 

 MADEREVA HAO WAPO KWENYE MAOMBI KABLA SHEREHE HAIJAANZA
 WA KWANZA KUTOKA KULIA NI MKE NA DEREVA ALIYESTAAFU MUDA WAKE WA KAZI PHED NDALE WA PILI KUTOKA KULIA NI PHED NDALE ANAYEAGWA WA TATU KUTOKA KULIA NI MGENI RASMI AFISA UTUMISHI WA HALMASHAURI HIYO FRANK EDGAR KOMBA NA WA NNE NI MWENYEKITI WA MADEREVA WILAYA YA NJOMBE PATRICK MFIKWA.
 MWENYEKITI WA MADEREVA WA SERIKALI WILAYA YA NJOMBE PATRICK  MFIKWA AKIMKARIBISHA  MGENI RASMI







Umoja Wa  Madereva  Wilayani Njombe Wametakiwa Kuzingatia  Sheria Na Kanuni Za Udereva Na Maadili Ya Kiutumishi  na kuvumilia vikwazo mbalimbali vinavyoweza kutokea  baina ya  wakuu wa idara na kuwasilisha malalamiko kwa mwajili wao.

.Rai hiyo imetolewa na afisa utumishi wa halmashauri ya Wilaya ya Njombe Frank Edgar  Komba wakati akiwa mgeni rasmi kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri hiyo katika hafra fupi ya kumuaga dereva Phed Ndale aliyestaafu kazi mwezi huu.

Bwana Komba amewasihi watumishi wastaafu kwamba wanatakiwa kwenda kuishi vizuri na jamii kama walivyokuwa wakiishi wakiwa kazini na kuiendeleza miradi iliyokwishaibuliwa  na siyo kutumia pesa za mafao ya kustaafu kuanzishia miradi mipya.

Akizungumza mbele ya wana umoja wa madereva hao  dereva aliyekuwa anaagwa  Bwana Phed Ndale amesema madereva wanaobaki wanatakiwa kuzingatia miiko ya kazi za kiutumishi ili wasifukuzwe kazi na kuacha ugomvi na wakuu wa idara pindi vikwazo vinapokuwa vinatokea.

Bwana Ndale Amesema Ameanza Kazi Serikalini Mwaka 1973 akiwa ametoka kufanya kazi kama kibarua kwa kipindi cha miaka 13 serikalini  na uvumilivu wake ndiyo uliomsaidia hadi kufikia kustaafu kwake.

Mwenyekiti wa umoja wa madereva kwa Halmashauri tatu za Njombe, Wanging’ombe na Makambako  Luka Malongo ametoa historia ya umoja huo  kwamba ulianzishwa mwaka 2013 wakiwa 32 baada ya kuambiwa wabadilishe leseni kwa lengo la kutatua changamoto mbalimbali za kila dereva na kusaidiana kwenye shida na raha huku mwenyekiti wa madereva Wilaya ya Njombe Patrick Mfikwa akisema umoja huo utaendelea kudumishwa.



No comments:

Post a Comment