Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Tuesday, August 9, 2016

HALMASHAURI WILAYA YA NJOMBE KUKARABATI KITUO CHA KUZUIA UPOTEVU WA MAZAO YA MBOGAMBOGA NA MATUNDA

 LUKELO MSHAURA AFISA HABARI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI NJOMBE

HIKI NDIO KITUO CHENYEWE CHA KUTOLEA MAFUNZO KWA WAKULIMA WILAYANI NJOMBE

Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Kupitia Programu Ya MIVARF Inakarabati Kituo Cha Mafunzo Ya Kuzuia Upotevu Wa Mazao Ya Mbogamboga Na Matunda    Lengo   Kuwezesha Wakulima   Kuzuia Upotevu Na Kuongeza Thamani Ya Mazao Na  Kipato  Cha Mkulima .

Afisa Habari Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe  Lukelo Mshaura  Amesema Kupatikana kwa mradi huo Kunatokana Na Jitihada Za Halmashauri  Hiyo   Kuandaa Maandiko Mbalimbali Ya Uwekezaji Wa Miradi Ya Maendeleo Kwa Lengo La Kusaidia Wananchi Na Kuongeza Mapato  Ya   Halmashauri.

Bwana Mshaura Amesema Mradi huo Unaofadhiliwa Na Programu Ya Mivarf Ni Muendelezo Wa Mradi Mwingine Wa Kuimarisha Zao La Mnyororo Wa Mahindi  kupitia taasisi ya Uongozi Na Maendeleo Ya Ujasiliamali  Unaotekekezwa Katika Vijiji 13 Kwa Kata Za Ninga, Ikuna, Na Kichiwa  Wilayani   Njombe.

Amesema Kazi Kubwa Inayofanywa Na MIVARF  Kwa Kushirikiana Na Halmashauri Ya Wilaya Ya Njombe Ni Kuwajengea Uwezo Wakulima Na Vikundi Vya Uzalishaji Ikiwemo AMCOS Na Kuwaunganisha Kwenye Masoko Kwa Zao La Mnyororo Wa Thamani Lililochaguliwa  Na Wadau Wa Kilimo Ambalo Ni Mahindi. 

Amesema Kituo Hicho  Kitakuwa Na Uwezo Wa Kuchukua Watu 40 Kwa Wakati Mmoja  Ukarabati  Wake Utaghalimu Zaidi Ya Shilingi  Milioni  74 , Unatekelezwa  Kwa Awamu Mbili , Ikiwemo  Ukarabati  Uliopo   Kukamilishwa Na Usimikaji  Mitambo Iliyopo  Kwenye Mchakato Wa manunuzi .

Amesema  Kituo Hicho   Kitahudumia  Wakulima , Mkoa Wa Njombe  Ambao  Wazarishaji Wa Mazao Ya  Matunda Na Mbogamboga Hususani  Nyanya  Na Kitatoa Fursa Kwa Vikundi  Kupata Mafunzo Ya Stadi Za Usindikaji  Mazao Na Kusaidia Kupunguza Upotevu  Wa Mazao Na Kuongeza Thamani  Na Kipato.


No comments:

Post a Comment