Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Sunday, August 7, 2016

SERIKALI YATENGA BAJETI YA SHILINGI MILIONI 800 KWAAJILI YA UKARABATI WA HOSPITALI YA KIBENA

 MBUNGE WA JIMBO LA NJOMBE MJINI EDWARD FRANZ MWALONGO AKIZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA WA NJOMBE MJINI
 KAMANDA WA POLISI MKOA WA NJOMBE PUDENCIANA PLOTAS AKIWA NA VIONGOZI WA WAFANYABIASHARA NJOMBE MJINI


 HAWA WAFANYABIASHARA WA NJOMBE WAKISIKILIZA KWA UMAKINI HOTUBA YA MBUNGE WA NJOMBE MJINI EDWARD FRANZ MWALONGO

 MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA NJOMBE  ONESMO BENEDICT WA KULIA AKIWA NA KAIMU WAKE WAKIJADILIANA JAMBO UKUMBI WA TURBO




 MWANYEKITI WA JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA MKOA WA NJOMBE ONESMO BENEDICT AKIZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA MBELE YA MBUNGE YEYE ANASEMA HUWA WANAOMBA KUKUTANA NA MKURUGENZI USO KWA USO NA MKURUGENZI LAKINI AMEKUWA AKIPIGA CHENGA SASA WANAHITAJI KUKUTANA NAYE WAFANYE MAZUNGUMZO JUU YA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI.

MWALONGO EDWARD  AKIWA UKUMBI WA TURBO NJOMBE MJINI

Serikali  Imetenga Kiasi Cha Shilingi Milioni Mia  Nane  Katika Bajeti Ya Mwaka 2016/2017 Kwaajili Ya Kukarabati  Hospitali Ya Mkoa Wa Njombe Kibena  Ambapo Ukarabati Wake Unatarajia Kufanyika  Mara Baada Ya Fedha Hizo Kufika   Ili Kupunguza Changamoto Ya Uchakavu Wa Miundombinu Mbalimbali Ya Hospitali Hiyo.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Mbunge Wa Jimbo La Njombe Mjini Edward Franz Mwalongo Wakati Akizungumza Na Wafanyabiashara  Wa Njombe Mjini  Na Kusema Kuwa Wafanyabiashara Wanatakiwa Kutambua Kuwa Serikali   Inamalengo Ya Kuboresha Miundombinu  Mbalimbali   Ya Kijamii Ikiwemo  Ukarabati Wa Sehemu Za Afya.

Aidha Mwalongo Amesema  Serikali Inaendelea Na Jitihada  Za Kupeleka Mradi Wa  Maji Katika Hospitali Ya Kibena  Ambapo Mradi Huo  Umedaiwa Utadumu Kwa Muda Wa Mwaka Mmoja Kukamilika Kwake  Na Kipaumbele  Cha Maji  Hayo Kufikishwa Kitakuwa Kwenye Hospitali  Na Eneo La Chuo Cha  Nurssing  Kibena.

Kwa Upande Wake  Mwenyekiti Wa Jumuiya Ya Wafanyabiashara Njombe Mjini  JWT  Onesmo  Benedict  Amesema Wafanyabiashara Hao Wanakabiliwa Na Changamoto Ya  Serikali  Kuwatumia Wafanyabiashara Wa Mikoa Ya Nje  Kusambaza  Vifaa  Vya Ujenzi Ikiwemo Saruji,Nondo Na Mali  Nyingine  Za Kujengea  Kutochukuliwa Njombe Licha Ya Badhaa Hizo Kuwepo Madukani.

Nao Wafanyabiashara  Waliokuwepo Kwenye Mkutano Huo  Wamelalamikia Kuwepo  Tatizo La  Uchafu Iliopo Kwa Baadhi Ya Maeneo  Na Kusema Wataalamu Wa Afya   Hakuna Kazi Wanayoifanya  Na Kumuomba Mbunge Kutilia Mkazo  Swala La Usafi, Uharibifu Wa Miundombinu Ya Barabara  Huku ZIlizolimwa Kutomwagiwa Maji.

No comments:

Post a Comment