.Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati)akipokea moja ya bati kutoka kwa Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni hiyo, Subash Patel ikiwa ni sehemu msaada wa
kupaulia vyumba madarasa leo jijini Dar es Salaa , Kushoto ni Katibu
Tawala wa Mkoa, Thelesia Mmbando.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiangalia mtambo wa kutibu maji
taka na kuweza kutumika katika matumizi mengine wakati alipotembelea
matambo huo katika kiwanda cha uzalishaji bati cha MMI Steel.
Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii
MKUU
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa wanaotoa misaada
haimaanishi kuwa wanataka kutengeneza mazingira ya kukwepa kodi,ni
wajibu wa kampuni au taasisi kuguswa kwa namna moja ama nyingine katika
kusaidia kutatua changamoto zinazoizunguka jamii .
Makonda
ameyasema hayo leo,wakati wa makabidhiano wa bati 10000,na madawati
1000, kutoka kwa kampuni ya kuzalisha bati ya MMI Steel na Baps Charity
amesema kuwa kampuni hiyo imefungua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya
madarasa.
Makonda
amesema kuwa Rais Dk. John Pombe Magufuli alitoa bilioni mbili hivyo
bati hizo zitakwenda katika kupaua vyumba vya madarasa na bati zingine
zitabaki hivyo wadau waitikie wito wa kujenga vyumba vya madarasa.
Amesema
kampuni hiyo imetoa sehemu yake katika kuunga mkono jitihada za Rais
Dk.John Pombe Magufuli ya elimu bure ambayo itaendana na mazingira bora
ya kusomea.
Makonda amesema kuwa kampuni hiyo imeweka mtambo wa majitaka kusafisha na kutumika tena na kutaka kampuni zingine zifanye hivyo.
Amesema kuwa wenye viwanda kuacha kutumia mitaro ya mvua kutiririsha maji na kutengeneza mifumo yao.
Nae
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Subash Patel amesema kuwa wameona
umuhimu wa elimu na jitihada za Rais na kuamua kutoa sehemiu ya uwezo
wao.Patel amesema kuwa wataendelea kutoa kadrichangamoto zinapoibuka.
No comments:
Post a Comment