Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Thursday, May 12, 2016

WAUGUZI WA HALMASHAURI YA MJI NJOMBE WAITAKA SERIKALI KULIPA FEDHA ZA LIKIZO KABLA YA KWENDA LIKIZO


 WAUGUZI WAKIWA KWENYE MAANDAMANO KUTOKEA HOSPITALI YA TANWAT KUELEKEA CHUO CHA WAUGUZI KIBENA








 MGENI RASMI KATIBU TAWALA MSAIDIZI GIDEON MWINAMI AKIPOKEA MAANDAMANO HAYO

 WAUGUZI WANAWASHA MISHUMAA YA ISHARA YA UPENDO


















 MGENI RASMI BAADA YA KUSIMAMA KUTOA HOTUBA YAKE





 WAUGUZI WAKIPELEKA ZAWADI KWA WAUGUZI WANAOTARAJIA KUSTAAFU


 RISALA YA WAUGUZI IKIWASILISHWA KWA MGENI RASMI LEO KATIKA UKUMBI WA CHUO CHA WAUGUZI KIBENA


 WAUGUZI HAPA WANAONESHA FANI YA KUIGIZA KWA NKUTOA HUDUMA KWA WAGONJWA WAKIWA MBELE YA MGENI RASMI


HUU NDIYO UKUMBI WA CHUO CHA UUGUZI KIBENA



Zaidi Ya Wauguzi 200  Wa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  Leo Wameungana Na Wauguzi Wengine 

Kuadhimisha Siku  Ya Wauguzi Duniani Kote  Ambapo  Katika Kuadhimisha Siku Hiyo  Wamefanikiwa

Kufikisha  Changamoto  Mbalimbali Ambazo Zimekuwa Zikiwakabili  Wauguzi Wakati Wa Kutekelez

Majukumu Yao Ikiwemo Kutopatiwa Mafao Ya  Kustaafu Kutoka Mashirika Ya Hifadhi Ya Taifa Ya Jamii.

Akizungumza Kwenye Maadhimisho Hayo Kwa Niaba Ya Katibu Tawala Mkoa Wa Njombe Jackson

Saitabahu,Katibu Tawala Msaidizi  Gideon Mwinami  Ametaka  Wauguzi Kuitumia Siku Hiyo Kwaajili Ya

Kukumbushana  Utekelezaji Wa Majukumu Yao Kwa  Uadilifu Na Kufuata  Misingi Ya Maadili  Ya Utendaji

Kazi Kwenye Vituo Vyao.

Kuhusu  Malalamiko Ya Wauguzi  Kutopandishwa Vyeo Na Kuongezewa Mishahara Pindi Wanapotoka

Masomoni  Katibu Msaidizi Huyo Mwinami  Ameahidi Kuzifikisha  Changamoto Hizo Kwa  Mkurugenzi  Wa

Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Ili Kutatua  Zile Zilizo Chini Ya Uwezo Wake Huku Akitaka Jamii

Kuwathamini Wauguzi  Hao  Kwa Kuonesha Ushirikiano  Wakati Wa  Kutekeleza Majukumu Yao.

Rustika Mtemba Ni Mwenyekiti Wa  Chama Cha Wauguzi  Halmashauri Ya Mji Wa Njombe  TANNA 

Ambaye Ametaka Serikali Kuwafikilia Swala La Kuwafanyia Mabadiliko Ya Kupandishwa Vyeo Na

Mishahara  Wauguzi Wanapotoka Masomoni  Huku Akitupia Lawama  Mifuko Ya Taifa  Ya Hifadhi Ya Jamii

 Ikiwemo NSSF  Kwa Kushindwa Kutoa Mafao Yao Kwa Wakati.

Katika Risala Ya Wauguzi  Kwa Mgeni Rasmi Iliyosomwa Na  Dativa Mwinuka Imeeleza   Kuwepo Kwa

Changamoto Ya Wauguzi Kutopewa Sale Za Kazi,Kutolipwa Fedha Za Likizo Kwa Wakati,Fedha Za Masaa Ya

Ziada  Ambapo  Wamefanikiwa  Kupunguza Vifo Vya Watoto Wachanga Na Watoto Chini Ya Miaka Mitano.

Kwa Upande Wao Wauguzi Wakizungumza  Mara Baada Ya Hotuba Ya Mgeni Rasmi  Wametaka Serikali Kuwaboreshea Mazingira Ya Kufanyia Kazi   Kwaajili Ya Usalama Wao   Ambapo Wametolea Mfano Hospitali Ya Kibena Ambayo Mazingira Yake Yanahatarisha Usalaama Wao Kwa Kukosa Uzio  Na Kutaka Kupewa   Malipo Ya Masaa Ya Ziada  Pamoja Na Malipo Ya Likizo  Yatolewe Kabla Ya Kwenda Likizo.

Maadhimisho Ya Siku Ya Wauguzi   Duniani Kwa Halmashauri Ya Mji Wa Njombe Yamefanyikia Katika

Hospitali Ya Kibena  Huku  Kwa Mkoa Wa Njombe Yakifanyikia Wilayani Makete Yakiwa Na Kauli Mbiu

Isemayo  Wauguzi Ni Nguvu Ya Mabadiliko  Ya Uboreshaji  Wa Mifumo Ya Afya.

No comments:

Post a Comment