Pages

CONTACT

0757092504/0678321772

Friday, May 13, 2016

BAADHI YA WANANCHI WA VIJIJI VYA MWILAVILA NA TAMBALANG'OMBE KATA YA MALANGALI WILAYA YA MUFINDI WALALAMIKIA KULAZIMISHWA KUWASHONEA WATOTO WAO FULANA ZENYE RANGI YA CCM













Serikali Wilayani Mufindi  Mkoani Iringa Imepiga Marufuku  Kuanzishwa Kwa Michango  Na Sale Za Shule Ambazo Haziridhiwa Na Wananchi  Ili Kuepusha Migogoro Isiyo Ya Lazima Baina Ya Walimu Na Wazazi  Na Kutaka Walimu Wote Wa Shule Za Sekondari Na Msingi Kutojihusisha Na  Kushika Fedha Za Michango Yoyote Ya Wananchi  Kwenye Shule Zao.

Kauli Hiyo Imetolewa Na Afisa Habari Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Mufindi   Ndimmyake Mwakapiso  Kufuatia Kuwepo Kwa Malalamiko Kutoka Kwa Wananchi Wa  Vijiji Vya  Mwilavila Na Tambalang'ombe  Kulalamikia  Uongozi Wa Shule Ya Msingi Ihanga Kuwalazimisha  Kushona Fulana  Za Wanafunzi Zenye Rangi Zinazofanana Na Za Chama Cha Mapinduzi.

Aidha Afisa Habari Huyo Bwana Mwakapiso Amemuagiza Mwalimu Mkuu Wa Shule Ya Msingi  Ihanga  Kata Ya Malangali  Jacob  Sanandala Kuacha  Mpango Huo Wa Kulazimisha Wazazi Kuwashonea Watoto Wao Fulana Hizo Ikiwa Wazazi Hawajaridhia  Huku Akitaka Walimu Wote Kufuata Miongozi  Ya Elimu Waliyopewa  Na Kusimamia Taaluma Shuleni.

Mwakapiso  Amesema  Michango Yote Itakayoanzishwa Kwenye Shule  Ni Lazima Ilidhiwe Na Wazazi   Na Kutaka Walimu Wakuu Wote Wawe  Makini Katika Kipindi Hiki Ambacho Rais Magufuri Amepiga Marufuku Michango  Yote Shuleni   Huku Akikili Kupata Taarifa Za Kuanzishwa Mpango Wa Fulana Hizo Mbele Ya Mkutano Ambao Baadhi Ya Wazazi Hawakuridhia  Na Kusema Sale Zinazotakiwa Ni Zile Zilizokuwa Zinatumika Zamani .

 Mwalimu Mkuu Wa Shule Ya Msingi Ihanga Kata Ya Malangali Jacob Sanandala  Ambaye  Amesema Anayeweza Kulizungumzia Tatizo La Kulazimisha Wazazi Kuwashonea Fulana Wanafunzi Wa  Shule Hiyo  Ni Halmashauri Ya Wilaya Ya Mufindi  Kwani Yeye Hana Mamlaka Yoyote Kulizungumzia Tatizo Hilo.

Awali Wananchi Wa Vijiji Vya Mwilavila Na Tambalang'ombe Wamelalamikia  Uongozi Wa Shule Ya Msingi Ihanga Ukiongozwa Na Mwalimu Mkuu  Wa Shule Hiyo Jacob Sanandala Kwa Kuwarudisha Nyumbani Watoto Kwa Kukosa Fulana  Zenye Rangi  Inayofanana Na Zile Za CCM  Licha Ya Kutoridhia Mpango  Huo MpyaWa Kuanzisha  Fulana Hizo.

No comments:

Post a Comment